• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

ALLIANCE ONE YAKABIDHI MADAWATI NA MRADI WA KISIMA VYENYE THAMANI YA MILIONI 79 SHULE YA MSINGI KINGOLWIRA

Posted on: May 27th, 2022

KAMPUNI ya Tumbaku ya Alliance One Tanzania (AOTTL) iliyopo Morogoro imemkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe. Albert Msando, Mradi wa kisima na Madawati 300 vyote vikiwa na thamani ya Milioni 79 kwa ajili ya Shule ya Msingi Kingolwira iliyopo Manispaa ya Morogoro.

Tukio hilo la hafla fupi ya makabidhiano ya vifaa hivyo limefanyika leo Mei 27/2022 katika Shule ya Msingi Kingolwira na kushuhudiwa na Viongozi mbalimbali kutoka Manispaa ya Morogoro pamoja na Viongozi wa Kata na Wazazi wa wanafunzi.

Msaada huo umekabidhiwa Mkurugenzi wa fedha , Festo Mwalonga, akimwakilisha Mkurugenzi wa Alliance One kwa Mkuu wa Wilaya ya Morogoro , Mhe. Albert Msando, katika halfa iliyofanyika Shuleni hapo.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo, DC Msando, amesema kwa upande wa mradi wa kisima utasaidia kutatua kero za maji shuleni pamoja na msaada wa madawati ambao utasaidia wanafunzi kukaa katika mazingira rafiki darasani.

DC Msando, amewapongeza Alliance One kwa kuwa karibu na Jamii jambo ambalo linapaswa kuigwa na Taasisi nyingine katika kurudisha gawio kwa jamii kama sheria inavyosema.

"Leo ndugu zetu wametukimbilia kutusaidia , na nimepata taarifa sio mara yao ya kwanza , niwaombe sana walimu endeleeni na moyo wa kufundisha kwani Serikali inaendelea kuweka mazingira rafiki lakini kwa Wazazi wote hakikisheni mnafunga mkanda kwa kushirikiana na waalimu ili kuhakikisha wanafunzi na watoto wenu wanafikia malengo waliojiwekea , suala la malezi  msiwaachie waalimu lazima mshirikiane kikamilifu kama mnataka matokeo chanya" Amesema DC Msando.

Mwisho, DC Msando, ameutaka Uongozi wa Shule hiyo kuhakikisha wanatunza vizuri misaada wanayopewa na wafadhili na kuiwekea miundombinu mizuri ili iweze kuwasaidia katika kizazi cha leo na kesho.



Naye Mkurugenzi wa fedha Kampuni ya Alliance, Festo Mwalonga, ameipongeza Serikali kwa kuweka Mazingira mazuri ya uwekezaji na ufanyaji wa biashara nchini , hatua ambayo imefanikisha Kampuni yao ya Alliance One kuweza kuona inatoa misaada kwa jamii ikiwemo kusaidiana na Serikali.

Aidha, Mkurugenzi huyo wa fedha , amevitaja vitu vilivyotolewa ikiwamo Madawati 300 yenye thamani ya Shilingi Milioni 27,092,800.00 na Mradi wa Kisima wenye thamani ya Shilingi Milioni 52.



Ikumbukwe kuwa Alliance One sio mara ya kwanza kuisaidia shule hiyo kwani mwaka 2013 ilisaidia Shule hiyo Ujenzi wa Madarasa 2 na madawati 70 huku wakiendelea kuwa wadau muhimu katika kusaidia nyanja ya elimu.





Naye Kaimu Mkurugenzi Manispaa ya Morogoro , Chausiku Masegenya, amewataka waalimu kuweka mikakati ya pamoja ili kuongeza viwango vya ufaulu na ameishukuru Alliance One huku akiwataka kutokata tamaa ya kuendelea kuwasaidia kwani bado shule hiyo imekuwa na changamoto nyingi zinazoikabili.

Kwa upande wa Diwani wa Kata ya Kingolwira, Mh. Madaraka Bidyanguze, amesema Aliance One wamekuwa karibu nao kwa kila jambo na wamekuwa wepesi wa kusikiliza matatizo yao pale wanapokwenda kuomba msaada.

Mhe. Bidyanguze, ameomba wadau wengine kujitokeza kwa ajili ya kushirikiana na Serikali hususani katika kusaidia jamii ikiwamo huduma za elimu na masuala mengine mengine ya maendeleo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa