Waheshimiwa Madiwani,viongozi wa CCM wilaya,wakuu wa idara kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro leo tarehe 24 Aprili,2025 wamefanya ziara ya mafunzo katika Jiji la Tanga,lengo ikiwa ni kujifunza mbinu mbalimbali za ukusanyaji mapato na namna bora ya kuboresha usafi wa mazingira.
Akizungumza wakati wa ukaribisho,Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Mhe,Abdulrahman Shillow ameupongeza uongozi wa Manispaa ya Morogoro kwa kuchagua Jiji la Tanga kuwa sehemu bora ya kujifunzia na kueleza kuwa katika eneo la mapato wanaendelea kuboresha ukusanyaji na wanatarajia kuwa kinara wa ukusanyaji katika majiji yaliyopo.
Aidha ameeleza katika upande wa usafi wa mazingira Jiji la Tanga limeendelea kushika nafasi ya kwanza kitaifa katika upande wa majiji ila wao bado hawajaridhika wanaendelea na kutoa elimu kwa wananchi kuwa na tamaduni ya kuwa wasafi kila wakati.
Naye Mstahiki Meya Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga ameushukuru Uongozi wa Jiji Tanga kwa kuwapokea na kueleza kuwa Manispaa ilikuwa ikikusanya Bilion 4 ila kwa hivi sasa inakusanya Bil 14 hivyo kuja kujifunza hii itaongeza ufanisi katika ukusanyaji mapato.
Ziara hiyo ilianza na kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano uliopo katika ofisi za Jiji la Tanga kwa kujadiliana mambo mbalimbali na Mstahiki Meya wa Jiji,Naibu Meya wa jiji,na wataalamu wa Jiji la Tanga.
Wakiwasilisha mada wataalamu wa Jiji la Tanga walieleza mbinu mbalimbali wanazotumia kukusanya mapato sambambana uibuaji wa vyanzo vipya vya kuiwezesha Jiji kupata mapato na namna bora wanayoitumia katika kusafisha na kuhifadhi mazingira.
Miongoni mwa miradi iliyotembelewa na wagenii hao ni Dampo la kisasa la Mpirani,Jengo la kitega Uchumi la Samia Business Center na kiwanda cha kutengeneza Tofli cha “BLOCK MACHINE” cha kampuni ya SILKANT kinachomilikiwa na Jiji la Tanga.
Ziara hiyo imefanyika kwa mda wa siku tatu kuanzia tarehe 24-26 Aprili 2025.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro
Anuani: 166 morogoro
Simu: 0232614727
Simu: 0734-039300
Baruapepe : info@morogoromc.go.tz
Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa