• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

BEGA KWA BEGA NA MAMA SAMIA YAADHIMISHA SHEREHE ZA MIAKA 59 YA MUUNGANO, MGANGA MKUU MANISPAA YA MOROGORO ATOA NENO.

Posted on: April 26th, 2023

TAASISI ya Bega kwa Bega na Mama Mkoa wa Morogoro ,imeadhimisha sherehe za miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa kushiriki katika michezo mbalimbali pamoja na kuzungumzia miradi ya maendeleo inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Maadhimisho hayo yamefanyika katika Viwanja vya michezo Shule za Msingi Msamvu A na Msamvu B Aprili 26/2023 ambapo Mgeni rasmi alikuwa Mganga Mkuu wa Manispaa ya Morogoro Dr. Charles Mkumbachepa.

Akizungumza na wananchi waliojitokeza katika maadhimisho hayo, Dr..Mkumbachepa, amewataka Wananchi wa Mkoa wa Morogoro kuzidi kudumisha amani na kufanya kazi kwa bidii ili kuleta maendeleo.

Dk.Mkumbachepa,amesema kuwa kila Mtanzania ana mchango wake katika kufikisha maendeleo ya miaka 59 ya Muungano huku amani ikiwa chachu ya mafanikio kwa miaka hiyo ya Muungano.

Aidha, amesema kuwa thathmini inaonesha jinsi gani Tanzania ilivopiga hatua, hivyo kuna kila sababu ya kujua ni mambo yapi yamefanywa na Serikali chini ya Uongozi wa Awani ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Hata hivyo, amewataka wazazi na walezi kulipa kipaumbele suala la malezi kwa watoto.

“Naomba sana suala la malezi mliangalie vizuri watoto walelewe kimaadili na viongozi kusimamia utunzaji wa mazingira” Amesema Dr. Mkumbachepa.

Mwisho, ameipongeza Taasisi ya Bega kwa Bega na Mama huku akiahidi Serikali kuendelea kuwapa ushirikiano pale wanapo hitaji kujua miradi inayotekelezwa kwa ajili ya kuisemea.

Naye Mratibu wa Maadhimisho hayo kutoka Taasisi ya BEGA KWA BEGA NA MAMA, Ruth Mateleka, amesema kwa kipindi cha miaka 61 tangu taifa lipate uhuru limepiga hatua kubwa na sasa hata wakati wa miaka 59 ya Muungano Maendeleo ni makubwa sana

“Tanzania imepiga hatua kwa kiasi kikubwa sana kipindi kile tulikuwa tunasafiri siku nzima kwa sababu ya barabara, lakini sasa hivi ni rahisi sana, lakini miradi mikubwa inataekelezwa kama mradi wa Umeme wa Mto rufiji, ujenzi Hospitali za Rufaa na Wilaya pamoja na Vituo vya afya, Ujenzi wa Madarasa , Wodi za wakina mama na watoto , ujenzi wa mradi wa treni ya Umeme SGR yote haya Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan ameyafanya kwa kwa kipindi kifupi akiwa madarakani ” Amesema Mateleka.


Katika maadhimisho hayo zawadi kemkem zilitolewa kwa wana michezo waliofanya vizuri pamoja na vyeti vya shukrani kwa Viongozi.

Katika Maadhimisho hayo, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alielekeza maadhimisho sherehe za miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yafanyike katika ngazi ya mikoa kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi.

Ikumbukwe kuwa Muungano wa Taganyika na Zanzibari uliasisiwa tarehe 26 Aprili, 1964 takribani miaka 59 iliyopita, na Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere, na Hayati Abeid Aman Karume.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa