• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC KILAKALA AAGIZA HALMASHAURI MORO DC NA MANISPAA YA MOROGORO KUTENGA MAENEO YA UWEKEZAJI.

Posted on: February 10th, 2025

MKUU wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Mussa Kilakala, ameagiza Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro na Manispaa ya Morogoro kutenga maeneo ya kutosha kwa ajili ya uwekezaji ikiwamo,maeneo ya kilimo na viwanda vitakavyowezesha kuwepo vitega uchumi vingi katika Wilaya ya Morogoro.

Kauli hiyo ameitoa Februari 10/2025 katika Kikao cha kawaida cha Baraza la Biashara Wilaya ya Morogoro kilichofanyika katika Ukumbi wa Savoy Manispaa ya Morogoro.

DC Kilakala, amesema , maeneo yoyote duniani hayawezi kupiga hatua kimaendeleo na kiuchumi bila viongozi kukaa pamoja kuweka mazingira ya uwekezaji ,hivyo ni muhimu mazingira yatengwe ili yaweze kusaidia kuinua uchumi wa Wilaya ya Morogoro pamoja na kipato cha mtu mmoja mmoja.



"Ili tufanye vizuri katika eneo hili la uwekezaji, tunatakiwa kuandaa kikosi kazi cha Baraza la biashara ambacho lengo ni kutengeneza mikakati ya kutangaza fursa za uwekezaji katika Wilaya yetu"Amesema DC Kilakala.



Naye Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA) Mkoa wa Morogoro Muadhini Mnyanza,amesema lengo la kikao hicho ni kujadili changamoto za mazingira ya biashara katika Wilaya na kuzipatia ufumbuzi.



"Baraza hili ni jukwa rasmi linalotoa fursa ya majadiliano kati ya Sekta binafsi na sekta za Umma, tunamshukuru Mwenyekiti wetu DC Kilakala,ametupa muelekeo naamini kama yale ambayo tumeyawasilisha yakitekelezwa tutakuwa mbali na wafanya biashara wetu watakuwa kwenye mazingira rafiki na tutaongeza wawekezaji na kuongeza pato la Wilaya pamoja na pato la mtu mmoja mmoja" Amesema Mnyanza.

Kwa upande wake Mkuu wa Divisheni ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Manispaa ya Morogoro,John Kilunge, amesema tayari Manispaa imeshatenga maeneo ambayo yatatumika kama vitega uchumi vya Manispaa.



Kilunge ,amesema kuanzia mwanzoni mwa mwezi Machi 2025,watayatangaza maeneo yote ya Vitega uchumi kupitia mabango ya barabarani pamoja na mitandao ya Kijamii na kuwa na Mkutano Mkubwa wa kutangaza maeneo ya vivutio vya utalii na maeneo ya uwekezaji.



Kwa upande wa Mwenyekiti wa Chama Cha Wachimba Madini Mkoa wa Morogoro, Omary Mzeru,amesema kama maeneo ya uwekezaji yakitangazwa pamoja na kuitangaza Sekta ya madini kwa kutengewa masoko ya uhakika Mkoa wa Morogoro utakuwa Mkoa tajiri sana nchini.



Mzee Mzeru,amesema Morogoro ni mkoa wa pili kwa upatikanaji wa Madini nchini lakini bado wanakosa masoko ya uhakika jambo linalrudisha nyuma soko la madini.



Mzeru,ameiomba Serikali kuangalia kwa jicho la tatu Soko la Madini Mkoa wa Morogoro ili wachimba madini waweze kunufaika zaidi na madini wanayochimba na kuongeza pato la Mkoa wa Morogoro.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa