• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC MSULWA AWAAMSHA WAIGIZAJI NA WASANII KURUDISHA HESHIMA YA MICHEZO WILAYA YA MOROGORO

Posted on: October 2nd, 2020

MKUU wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Bakari Msulwa, amewata Wanamichezo na Wasanii waamke kwani huu ni muda muafaka wa kurudisha heshima ya Michezo katika Wilaya ya Morogoro.

Kauli hiyo ameitoa leo Oktoba 02,2020 kwenye kikao cha kukutana na wadau wa Michezo, Sanaa, Elimu na Mazingira Manispaa ya Morogoro kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Manispaa kwa ajili ya kujadili changamoto zinazozikumba sekta hizo.

Akizungumza na Waandishi wa habari, DC Msulwa, amesema lazima Morogoro isimame na kurudisha heshima yake katika Nyanja ya michezo, sanaa na utamaduni .

Msulwa, amesema anataka Morogoro ya Viwango katika michezo hivyo ni ngumu kuipata Morogoro ya Viwango kama huwezi kujua changamoto zake za kuanzia.

“Hiki ni kikao muhimu sana, tunahitaji kurudisha heshima ya Morogoro katika Sanaa na Michezo, tunaamini Morogoro ina vipaji vingi sana na asilimia kubwa ya wachezaji wametoka Morogoro , tulikuwa na timu nzuri sana lakini leo tumebakiwa na timu moja Mtibwa Sugar lazima tujiulize ni wapi tumekosea ili tuanze na hapo, tunaamini tukishirikiana kwa pamoja Morogoro ya Viwango inawezekana”” Amesema DC Msulwa.

Mwisho. Amechukua nafasi ya kuwakaribisha wanamichezo wote , Wananchi, Vikundi vya Michezo ikiwamo jogging, Watumishi wa Umma na binafsi katika Mkutano wa kujadili changamotoz a Wanamichezo na Wasanii ambapo kabla ya mkutano huo kutakua na mbio fupi zitakazooongozwa na Jogging kuanzia mishale ya saa 12:30 asubuhi kwenye Viwnaja vya Shule ya Msingi Mwere hadi Uwanja wa Mpira wa Miguu wa Jamhuri ambapo Mkutano huo utafanyika .

Kwa upande wa Msanii wa filamu na maigizo , Haviti Makoti, amemshukuru Mkuu wa Wilaya ya Morogoro huku akisema mpango aliouanzisha unalenga kuwajengea uwezo wasanii pamoja na Wananmichezo ili kutengeneza ajira kupitia tasnia ya filamu na michezo kwa ujumla.

Aidha, Makoti, amesema kuwa Wasanii wengi wa filamu Morogoro wamekuwa wakicheza filamu zao nje ya Morogoro na kwenda Jijini Dar Es Salaam, kutokana na Morogoro kuwa na shida ya kukuza vipaji vya sanaa jambo ambalo limekuwa likidumaza sanaa za waigizaji hao kutofikia malengo.

Hivyo, kwa niaba ya wasanii wenzake ,wamemuomba Mkuu wa Wilaya kuwaongezea nguvu ikiwamo kutafuta wadau ili waweze kusaidiwa kazi zao za sanaa katika kukuza vipaji na kujipatia kipato kama njia moja wapo ya ajira na kujikomboa na umasikini.

Kwa upande wa mchangiaji , Kitutu Mshana, ameshauri kuwepo na Makongamano ya kimichezo na sanaa ambayo yatawajumuisha Wanamichezo wote wanaotokea Morogoro pamoja na wasaanii ili fedha zinazopatikana ziende kusaidia kuchangia huduma shuleni ikiwamo vitabu na madawati n.k.

Kitutu ,amesema ili michezo iwe endelevu haipaswi ikawa siku moja pekee ipo haja ya watumishi kukutani mishale ya jioni kufanya mazoezi ambapo kupitia wao wanaweza kukutana na kujadili masuala mbalimbali ikiwamo kuanzisha michango mbalimbali itakayoweza kusaidia kunyanyua michezo na sanaa katika Wilaya ya Morogoro.

Naye msanii Mwasity Juma, amemuomba Mkuu wa Wilaya kuweza kusapati michezo hususani katika suala zima la mitaji kwani wana uwezo wa kuandaa mipango mizuri ya kisanii kama matamasha lakini changamoto inakuwa ni ukosefu wa fedha za kutangaza matamasha hayo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa