• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC MSULWA AWATAKA WATUMISHI KUFANYA KAZI KWA UADILIFU

Posted on: June 25th, 2020

MKUU wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Bakari Msulwa , amewataka watumishi wa umma Wilaya ya Morogoro kufanya kazi kwa weledi na uadilifu na kuwaasa wasikimbie maeneo yao kazi badala yake wawe chachu ya mabadiliko na utatuzi wa changamoto wanazokutana nazo katika maeneo yao.

Hayo ameyazungumza leo Juni 25,2020 wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya Ofisi dhidi ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya Mstaafu wa Morogoro, Mhe. Regina Chonjo kwenye ukumbi wa Mikutano wa Manispaa ya Morogoro.

Msulwa, amesema watumishi wa umma wana maarifa hivyo wanapaswa kutumia maarifa hayo kukabiliana na changamoto zinazowakabili badala ya kuhama maeneo ya kazi kwa kuwa Wananchi wanawahitaji kwa ajili ya kuwapa huduma wanazostahili.

Amesema vyema kila Halmashauri kujiwekea utaratibu wa kuwapongeza watumishi wanaotimiza wajibu wao vizuri ili kuongeza morali ya utendaji kazi kwa watumishi na kwa wale wanaokiuka maadili ya utumishi na kuwa wazembe katika kazi kupewa onyo kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa Umma.

“Utumishi wa umma ni fursa, utumishi wa umma ni fursa fanyeni kazi kwa weledi, uadilifu na ubunifu maana dunia inabadiilika na ndiyo maana tunasisitiza waajiri watoe mafunzo ya mara kwa mara ili watumishi waendane na mabadiliko ya sayansi na teknolojia,niwaombe muepuke uwizi na mfanye kazi kwa uadilifu wa hali ya juu na kuacha kufanya kazi kwa maigizo lakini haya yote yatakuja endapo tutafanya kazi kwa ushirikiano ” Amesema Mhe. Msulwa.

Aidha, amewakumbusha watumshi wa umma muelekeo wa serikali ya awamu ya tano katika kujenga misingi ya utumishi wa umma.

Amesema kuwa serikali inatarajia kuwa na watumishi wenye uadilifu uliotukuta katika jamii na utoaji huduma kwa wananchi, watumishi wanaowajibika kwa serikali nawananchi, nidhamu ya kazi kufanya kazi kwa juhudi na maarifa, ndio dira ya serikali na itasimamia kuona kuwa utekelezaji unafanyika.

""Kila mmoja atimize wajibu wake, migogoro kwa kiasi kikubwa inazuirika kwani Serikali yetu ina mfumo mzuri kuanzia ngazi za chini hadi za juu, baadhi ya wataalamu wanakuwa vyanzo vya migogoro huku wananchi wakihangaika bila sababu , lakini pia wananchi hawapewi taarifa kwa wakati hili sio jambo jema, kiongozi mzuri ni yule aliye katika suluhu ya matatizo na sio sehemu ya matatizo, niwaombe wataalamu msisubiri viongozi wa kisiasa waje watatua kero hizo fanyeni kazi na muwe makini katika kutatua migogoro kwa kutumia taaluma zenu ili wananchi muwape huduma bora na wafurahie matunda ya kuwa na Uongozi katika sehemu husika " Ameongeza Mhe. Msulwa.



Hata hivyo, amesema kuwa ni jukumu la kila mkuu wa Idara na kitengo kusimamia sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa umma ili kuweza kuleta maendeleo chanya kwa watu anawasimamia na kuondoa kero na malalamiko yanayojitokeza mara kwa mara kwani kuna matatizo mengine ni madogo ambayo yako ndani ya uwezo wa mkuu wa idara au kitengo kuweza kuyatatua.

Alimalizia kwa kuwapongeza watumishi wa Halmashauri ya Morogoro kwa uwajibakaji na utendaji wao kazi uliotukuka na kuwataka kuendelea na moyo huo huo wa kuwatumikia wananchi wa Manispaa ya Morogoro ili kuweza kuleta maendeleo kwa wananchi kuloingana na sekta zao.

Kwa upande wa Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Michael Waluse, amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa nasaha yake pamoja na maagizo kwa Watumishi wa Umma katika kutekeleza majukumu yao katika maeneo yao ya kazi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa