• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC NSEMWA AFUTURISHA, AHIMIZA WANANCHI KUDUMISHA AMANI NA UPENDO

Posted on: April 18th, 2023

MKUU wa Wilya ya Morogoro, Mhe.Rebecca Nsemwa, amewataka Wananchi hususani wa Wilaya ya Morogoro, kuendelea kudumisha upendo, umoja na mshikamano ikiwemo kufanya kazi kwa bidii.

Kauli hiyo ameitoa Aprili 18/2023 katika Ukumbi wa DDC Mbaraka Mwinshehe wakati wa hafla fupi ya kufuturisha wananchi pamoja na waumini wa Kiislamu .

Akizungumza na Wananchi hao waliojitokeza katika iftari hiyo, DC Nsemwa,amewataka wananchi kudumisha amani na upendo huku akiwasititiza kuachana na tabia ya ubaguzi.

DC Nsemwa, amewapongeza Wananchi wote waliojitokeza katika iftari hiyo aliyoiandaa , huku akiahidi kuwa serikali itaendelea kushirikiana na Dini zote katika kudumisha amani na upendo na kuwaletea wananchi maendeleo.

Hata hivyo, DC Nsemwa, ametoa wito kwa viongozi wa vyama vya siasa, dini na wanachi kwa ujumla kudumisha amani na utulivu uliopo bila kujali tofauti za itikadi zao, dini au makabila yao.

“mashujaa wetu wakati wakiipigania amani ya nchi yetu hawakuangalia vyama vyao, wala dini zao, walichojali ni utanzania wao na ndiyo amani tunayojivua hadi hii leo, hivyo naomba amani tuliyonayo Watanzania tusiitie doa, tuendelee kuing'arisha kwa upendo wetu na mshikamano wetu "Amesema DC Nsemwa.

Pia ametaka kuwe na vyombo vya kuleta matumaini kwenye jamii badala ya kukatishana tamaa na kukimbilia mambo yanayoashiria uvunjifu wa amani.

Aidha, DC Nsemwa , ametuma salamu ya heri ya Sikuuu ya Eid kwa wananchi wote na waumini wa Kiislamu wa Wilaya ya Morogoro, huku akiwaomba waendelee kufuata misingi ya dini na kudumisha upendo katika kuendelea kuiweka Wilaya ya Morogoro katika taswira nzuri pamoja na kuleta maendeleo na ustawi kwa taifa.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro , Ally Machela, amewahakikishia wananchi wa Manispaa ya Morogoro kuwa atasimamia kwa nguvu zote masuala yote yanayohusu maendeleo ya Manispaa ya Morogoro ikiwemo kudumisha mshikamano , upendo na amani kwa faida ya wananchi wote wa Manispaa ya Morogoro.

Machela , amesema kuwa sehemu ambayo hakuna amani basi hata utulivu wa maendeleo unakosekana.

Aidha, amesema kuwa amefurahishwa sana na mshikamano wa Madiwani wa Manispaa ya Morogoro kwa kuwa na dhamira ya pamoja ya kujadiliana mambo yenye maslahi mapana ya Manispaa ya Morogoro kwa kusimamia kikamilifu Ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM ya mwaka 2020-2025.




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa