• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DIWANI MWAMNYANYI AWATAKA WAZAZI KULEA WATOTO KWENYE MAADILI

Posted on: May 17th, 2023

DIWANI wa Kata ya Bigwa Manispaa ya Morogoro, Mhe. Melchior Mwamnyanyi, amewataka wazazi na walezi Kata ya Bigwa kuwalea watoto wao katika maadili mazuri yenye kulinda mila na desturi ili kuendeleza utamaduni wa kitanzania.

Kauli hiyo ameitoa Mei 16/2023 katika maadhimisho ya Siku ya familia duniani yaliyofanyika Ukumbi wa mikutano wa Ofisi hiyo.


Mhe. Mwamnyanyi, amesema wazazi na walezi wanawajibu mkubwa wa kuwafundisha watoto wao maadili yanayofuata misingi ya Nchi ili kuthibiti wimbi la mmomonyoko wa maadili katika kizazi hiki.

Aidha, amesema kuwekeza kwenye uhifadhi wa tamaduni, mila na desturi za asili inasaidia kuimarisha utulivu na amani ya Nchi ikiwa ni pamoja na kuzuia migogoro mbalimbali kwenye jamii.

"Niwaombe sana wazazi tuwekeze kwenye malezi na makuzi ya mtoto yanayohifadhi utamaduni wa asili ili kulinda mila na desturi za kitanzania, kufanya hivyo itasaidia watoto kukua katika maadili mema yanayozingatia utamaduni, mila na desturi za makabila yao katika mavazi, heshima na mambo mengine muhimu, na katika vikao wenyeviti ukatili wa kijisnia iwe agenda yenu "Amesema Mhe. Mwamnyanyi.


Pia Mhe. Mwamnyanyi, amesisitizia wazazi na walezi kuwalea watoto katika misingi ya kidini kwa kuhakikisha watoto wanakua katika maadili mazuri yanayozingatia utaratibu wa Nchi ili kutengeneza Taifa bora.



Naye Mtendaji wa Kata ya Bigwa, Helena Mgala, amewataka wazazi kushiriki kikamilifu katika kuhakikisha watoto wanapata malezi bora.



Naye Chediel Senzighe kutoka Kituo cha msaada wa kisheria (Morogoro paralegal Centre), amesema zipo sheria ambazo zinawaweka hatiani watuhumiwa wamasuala ya ukatili wa Kijinsia ambapo amewataka wazazi kutoa taarifa wanapoona mambo hayo yametokea kwa kuanzia ngazi ya Mitaa hadi Dawati la Polisi ili watuhumiwa kuchukuliwa hatua za kisheria.

kwa upande wa Wazazi , wametumia nafasi hiyo kuishauri serikali kusimamia sheria na sera zinazomhusu mtoto ili kuhakikisha hazileti athari katika makuzi yake.

Wazazi hao, wamepongeza juhudi mbalimbali za serikali zinazofanywa kimkoa na kitaifa kuanza uwekezaji wa makumbusho yanayohifadhi utamaduni wa asili ili kudumisha mila na desturi.

Aidha wazazi hao wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuimarisha utamaduni wa Nchi ikiwa ni pamoja na kutangaza utalii ambapo maeneo mbalimbali ya asili katika jamii yanafikiwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa