• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

HALMASHAURI YA MANISPAA YA MOROGORO IMEJIPANGA KUTUMIA KIASI CHA SH BIL.75.4 KWA MWAKA WAFEDHA 2018-2019

Posted on: January 8th, 2018

HALMASHAURI ya Manispaa ya Morogoro imejipanga kutumia kiasi cha sh.Bil.75.4 kutoka vyanzo vyake mbalimbali ikiwemo mapato ya ndani na fedha kutoka kwa wahisani kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2018-2019.

Hayo yalibainishwa  na Mchumi wa Manispaa ya Morogoro Ndg Sadoth Kaijage kwenye kikao cha bajeti cha kamati ya ushauri ya Wilaya kilichofanyika mjini hapa.

Kaijage alisema kuwa kwa kipindi cha mwaka mwaka wa fedha 2018-2019 Halmashuari inakisia kupokea kiasi cha ruzuku na kukusanya mapato ya ndani ya kiasi cha Sh. Bil. 75.4 kutoka vyanzo vya Halmashauri,serikali kuu,matumizi ya kawaida ,wahisani na uchangiaji wa huduma za afya.

Aidha alisema kuwa katika bajeti hiyo Halmashauri imezingatia mpango wa maendeleo wa Taifa,kusikiliza maoni ya wadau mbalimbali ,mpango wa lishe na dira ya maendeleo ya taifa ya mwaka 2020 -2025 ili kuhakikisha bajeti hiyo inamletea tija mwananchi.

Awali Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Morogoro Ndg.Yahaya Nania akifungua kikao hicho kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro alisema kuwa rasimu ya mapendekeo ya bajeti ya mwaka 2018-2019 imezingatia sheria ya bajeti namba 11 ya mwaka 2015 pamoja na ilani ya Chama cha Mapinduzi.

‘’Pia bajeti hii imezingatia maelekezo mbalimbali kutoka Wizara ya fedha na nyinginezo’’alisema Nania.

Kwa upande wake mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro John Mgalula alisema kuwa tayari halmashauri imeweka mikakati mbalimbali ya ukusanyaji wa mapato katika kipindi hiki cha mwaka 2018 -2019 ili kuweza kuongeza mapato yake ya ndani.

Mgalula alitaja baadhi ya mikakati hiyo kuwa ni pamoja na kupitia upya mfumo wa usimamizi na ufuatiliaji wa mapato kwa kuboresha maeneo ambayo yana upungufu ,kuendelea kuwashirikisha wadau ,kutoa elimu kwa walipa kodi pamoja na kufanya kaguzi mbalimbali ili kubaini mianya inayovujisha mapato.

‘’Mkakati mingine ni pamoja na kubinafsisha baadhi ya vyanzo vya mapato kama vile ushuru wa mabango pamoja na utumiaji wa mfumo wa kielektroniki katika vyanzo vyote vya mapato ya ndani.’’alisema Mgalula.

Hata hivyo Mkurugenzi alisema Halmashauri imeweka kipaumbele katika ukusanyaji mapato,usafi wa mji ili kuweza kufikia lengo la kuwa jiji ,utawala bora ,afya ,maji ,ujenzi na uendelezaji wa viwanda.




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa