• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

KAGAMBO AWAASA WAMILIKI WA VITUO VYA MAKUZI NA MALEZI WA WATOTO KUVISAJILI.

Posted on: July 1st, 2022

KATIKA kuhakikisha watoto wanapata huduma za malezi, Makuzi na Maendeleo ya awali kadiri ya taratibu za serikali , Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Manispaa ya Morogoro, Hamisa Kagambo,amewataka Wamiliki kukamilisha taratibu za usajili ili Vituo hivyo visajiliwe.

Akizungumza na wamiliki wa vituo vya makuzi na malezi kwa watoto wachanga na watoto wadogo,Kagambo, amesema kikao hicho, kina lengo la kusaidia uboreshaji wa huduma kwa watoto vituoni ikiwepo wamiliki kuendelea kufanya usajili wa vituo, kwani kwa kufanya hivyo kunaongezea thamani vituo hivyo na kuvifanya vitambulike rasmi kisheria.



Kagambo amesema, watoto kuwepo katika vituo hivyo kunasaidia ulinzi na usalama wa watoto, kuwepo kwa ujifunzaji wa awali kwa watoto na wazazi /walezi wanapata muda wa kufanya shughuli za kiuchumi.





Amesema usajili wa vituo hivyo ni bure kwani sheria ya mtoto namba 21 ya Mwaka 2009 kifungu cha 147 mpaka 152 na kanuni za watoto imetoa ufafanuzi kuhusu vituo vya kulelea watoto wadogo na watoto wachanga mchana na imeeleza taratibu za kufuata wakati wa kufungua vituo vya makuzi na malezi kuwa na vigezo vinavyohitajika.



" Manispaa ya Morogoro tuna jumla ya vituo 103 vinavyojulikana na ustawi wa jamii kati ya hivyo vimesajiliwa vituo 25 na vituo 5 vipo katika mchakato , hivyo ni vema kwa kila anaeanzisha vituo avisajili kwanza kwaajili ya kumlinda mtoto" Amesema Kagambo.



Naye, Mwenyekiti wa umoja wa wamiliki wa day care centers -Manispaa ya Morogoro (UWADAMO), Clarence Burchard Mkwama ambaye ndiye mmiliki wa Mary Children Day Care Sabasaba, ameipongeza idara ya Ustawi wa jamii kwa kusimamia UWADAMO na kuepelekea kuongeza uelewa kwao na kuanza kufanya mabadiliko chanya ya kutoa huduma za vituo kwa watoto na kuwepo na umoja huo utawasaidia kujadiliana na kupeana uzoefu katika eneo la huduma vituoni.



Upande wa Katibu wa UWADAMO, Bi. Mary Kessy,ambaye ndiye mmiliki wa St.Maria Consolata SUA, amesema serikali na wadau wasichoke waendelee na jitihada hizo na ikiwezekana kutoa mafunzo hadi kwa wazazi/walezi yawafikie ingawaje pia wao kama wamiliki na walezi vituoni watasaidia kutoa elimu ya malezi kwa wazazi/ walezi katika vituo.



Kwa upande wa Mwakilishi wa wamiliki kutoka Hittler Day Care , ameushukuru Uongozi wa UWADAMO, kwa kushirikiana na Manispaa ya Morogoro katika kutoa elimu na kupelekea kusaidia uundaji wa umoja wa wamiliki wa day care centers -Manispaa ya Morogoro ambapo Umoja huo umekuwa msaada wa kuongeza ujuzi kwa wamiliki na walezi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa