• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI MANISPAA YA MOROGORO YAFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA MIRADI YA UJENZI WA SOKO KUU LA KISASA NA UJENZI WA STENDI MPYA YA DALADALA.

Posted on: November 14th, 2019

KAMATI ya Fedha na Uongozi  Halmashauri  ya  Manispaa yav Morogoro leo Novemba 14, 2019, imefanya ziara ya kutembelea miradi  inayotekelezwa ndani ya manispaa, ikiwemo mradi wa  Ujenzi wa Soko kuu la kisasa Kata ya Mji Mkuu, pamoja na mradi wa Ujenzi wa Stendi mpya ya Daladala iliyopo Kata ya Mafiga.

Akizungumza na Waandishi wa habari, Mstahiki Meya wa  Halmashauri ya Manispaa ya  Morogoro, Mhe. Pascal Kihanga, amesema lengo la kutembelea miradi hiyo ni  pamoja na kuangalia maendeleo ya miradi hiyo ilipoishia na inavyoendelea.

Aidha, Meya Kihanga, amesema katika ziara hiyo wamebaini kutokuwepo na kasi nzuri ya ujenzi japo maendeleo yake yanaridhisha, hivyo ametoa agizo kwa wakandarasi wanaosimamia miradi hiyo wafanye kazi usiku na mchana ili miradi hiyo ikamilike kwa wakati na kuwahudumia wananchi.

Katika upande wa mradi wa kimkakati uliopatiwa ruzuku na Serikali kuu, Mhe Kihanga, amemtaka mkandarasi kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati kwa ajili ya kuwawezesha wananchi  kupata huduma  bora za kiuchumi na kijamii.

Amesema matarajio yake katika mradi huo ni kwamba hadi kufikia Desemba 31 , mwaka huu 2019 , mradi huo utakuwa umekamilika.

Amesema mradi huo pindi utakapokamilika utawahudumia zaidi ya wafanyabiashara 1500, huku kipaumbele cha kupewa maeneo ya biashara kitatolewa kwa wafanyabiashara waliokuwa wanafanya biashara awali kabla ya soko la zamani kuvunjwa.

" Mhandisi tunakwama wapi? unajua wakati Naibu Waziri wa fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, alipofanya ziara hapa tulikuwa katika kasi kubwa sana, nashangaa sasa hivi kasi ya ujenzi imepungua, sasa hebu tushirikiane Mkandarasi, mtaalamu mshauri wa mradi pamoja na Manispaa tuwe kitu kimoja , tunapo kwama tuambiane na kama kuna shida ya fedha ziombeni kwani pesa zipo zinatusubiria sisi na ikifika desemba 31 hizi fedha zitaondoka na tutazikosa , sitaki tuzikose maana zikiondoka nyinyi wakandarasi mtakosa fedha na sisi tutakosa fedha na tutakuwa tumekwamisha huu mradi unaotegemeawa kutoa huduma kubwa na kuingizia pato taifa pamoja na Manispaa yetu" Amesema Mhe. Kihanga

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, amesema wataendelea na ziara za kutembelea miradi hiyo mara kwa mara kwani miradi hiyo imetengwa kwa lengo la kuifanya mamlaka za Serikali za Mitaa za  Manispaa ya Morogoro ziweze kujitegemea kimapato.

Aidha amesema mradi huo utagharimu Shilingi Bilioni 17,ambapo pindi mradi huo utakapokamilika Halmashauri inategemea kukusanya takribani kiasi cha Shilingi Bilioni 2.7 kwa mwaka hivyo itapunguza kutegemea ruzuku toka Serikali kuu.

Licha ya kuridhishwa na  hatua za mradi huo iliyofikiwa katika utekelezaji   aliwataka wale wote wanaosimamia mradi huo kuzidisha kasi ya ujenzi, na kuona mkandarasi anakuwa site masaa ishirini na nne kuhakikisha ujenzi huo unakamilika kwa wakati na kuzuia upotevu wa fedha za wanyonge zinazotekeleza mradi huo.

Kwa upande wa Mhandisi wa Manispaa ya Morogoro, Eng. Juma Gwisu, amesema ujenzi huo mpaka sasa umefikia asilimia 75%, na wanatarajia kukamilisha mwishoni mwa mwaka huu Desemba 31.

Mwenyekititi wa Mipango Miji na Diwani wa Kata ya Mwembesongo, Ally Kalungwana , amesema wao kama Kamati ya fedha na uongozi, hawatachoka kufanya ziara hizo kwani kufanya ziara hizo kunasaidia miradi mingi kwenda kwa kasi

Naye Kelvin Chacha, msimamizi wa mradi, amesema kuchelewa na kusua sua kwa mradi huo kumetokana na changamoto zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wa mradi ambazo ni kuwepo kwa mtandao wa maji taka ,uwepo wa wingi wa maji eneo la maradi (High table) uvunjaji wa misingi ya majengo ya soko la zamani, pamoja na mvua zilizonyesha kipindi cha hivi karibuni.

Katika hatua nyengine, Mhandisi wa Mkandarasi wa Kampuni ya Ujenzi ya Nadra Engineering Construction Company Ltd, Charles Richard, amesema ujenzi huo utakuwa na Maduka 304, Meza 900, maeneo makubwa 16 ya kupangishwa kwa mita za mraba (benki, maduka makubwa na ofisi ) maegesho ya magari makubwa 5 ya mizigo kwa pamoja, maegesho ya magari madogo 143 kwa pamoja, vyoo, migahawa, stoo 36 za mitumba, bucha pamoja na eneo la kuchinjia kuku.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa