• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

KATA YA BOMA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI KWA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA KATIKA MAENEO YA UMMA NA SERIKALI

Posted on: March 2nd, 2023

KATA ya Boma Manispaa ya Morogoro imeadhimisha Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Wanawake duniani kwa kufanya usafi.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Afisa Mtendaji Kata ya Boma, Prisca Mawala, amesema lengo la kufanya usafi ni kujikinga na magonjwa ya milipuko na yanayosababishwa na mazingira ya uchafu ukiwemo ugonjwa wa Kipundupindu,kuhara na Malaria.

“Leo sisi wanawake wa Kata ya Boma tumeadhimisha siku ya wanawake duniani kwa kujitokeza kufanya usafi katika eneo letu la Ofisi ya Kata, eneo la Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya ghorofa, kwenye mitaro pamoja na eneo la Kituo cha Polisi Kata ambapo ujenzi unaendelea, lengo la usafi ni kuonyesha mfano na kuwahamasisha wakinamama wenzetu kufanya usafi kwa kujitolea wenyewe bila ya kushurutishwa ili kujiepusha na magonjwa nyemelezi na milipuko kama ugonjwa wa kipundupindu,kuhara hata na Malaria yanayotokana na wadudu wanaozaliana sehemu za mitaro isiyotembea na takataka zinazokaa kwa muda mrefu hivyo tumejitolea leo kufanya usafi ili tuwe mfano wa kuigwa lakini pia kumuunga mkono Rais wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kampeni ya usafi " Amesema Mawala.

Mawala, amesema kuwa wanaendelea kuhamasisha wananchi kufanya usafi katika mazingira yanayowazunguka lakini pia ni wajibu kwa kila mtu kufanya usafi katika eneo lake pamoja na kutosahau siku ya juma la mwisho wa mwezi lililowekwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan la kufanya usafi katika mazingira yao.

Katika hatua nyingine, Mawala, amempongeza Diwani wa Kata ya Boma licha ya kutokuwepo lakini asilimia kubwa ya maandalizi ya shughuli hiyo Mhe. Diwani ametoa nguvu yake ya kufanikisha maadhimisho hayo.







Naye Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Boma, Bi. Fitina Mhina,amesema kuwa amesema kuna baadhi ya wananchi hata wakinamama wamekuwa wagumu wa kushiriki kufanya usafi katika mazingira yao kutokana na hali jinsi ilivyo kuwa ngumu wanakuwa wanajikita kufanya biashara zao ili wajipatie kipato lakini wao kama wakinamama watawashauri wapange siku katika wiki wafanye usafi kwenye mazingira yao yanayowazunguka.


Bi. Fitina,amempongeza Afisa Mtendaji wa Kata ya Boma pamoja na watendaji wenzake kwa kuja na mpango wa kufanya usafi katika maadhimisho hayo.

Elimu iyotolewa katika maadhimisho hayo ni elimu ya kupinga vita dhidi ya ukatili wa kijinsia, ulinzi wa watoto pamoja na uundaji wa vikundi na mikopo ya wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa