• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MBUNGE MZERU AAHIDI MILIONI 1.5 KUTUNISHA MFUKO WA JUKWAA LA WANAWAKE KIHONDA KUJIKWAMUA KIUCHUMI.

Posted on: March 7th, 2023

MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Morogoro, Mhe. Norah Mzeru, ameahidi kuwapatia Jukwaa la Wanawake Kata ya Kihonda Shilingi milioni 1 na laki 5 kwa ajili ya kutunisha mfuko wa jukwaa lao katika kujikwamua kiuchumi.

Ahadi hiyo ameitoa Machi 04/2023 akiwa mgeni rasmi katika sherehe za maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Kata ya Kihonda.

Akizungumza na Wanawake hao, Mzeru, amesema lengo ni kuona wanawake wanafanikiwa na kusonga mbele.

Kuhusu mradi wa uchakataji wa Chupa za plastiki, Mhe. Mzeru, ameahidi kuwapa shilingi Milioni 1 kwa ajili ya kuongezea katika ununuzi wa mashine ya uchakataji huku akisema shilingi laki 5 zitaingia kama mchango wa kutunisha mfuko wa Jukwaa kwani anafahamu malengo waliyokuwa nayo wakina mama hao.

"Nimeguswa na miradi yao hususani huu wa uchakataji chupa za plastiki, nimeahidi kuwapa milioni 1 waongeze katika ununuzi wa mashine hiyo, lengo ni kuona wakina mama Kihonda wanakuwa ni wa mfano Kimkoa kuweza kuwa na kiwanda kitakachowasaidia kujiari na kupata mapato” Amesema Mzeru.

Mzeru ,amesema Kiwanda hiko cha uchakataji kitachangia kutoa mchango mkubwa wa kuinua uchumi wa akina mama wa Kihonda na kutoa ajira kwa wengine.

Aidha, amesema mradi huo wa uchakataji chupa za plastiki ni hatua ya utekelezaji wa Ilani ya CCM na pia kuunga mkono juhudi za Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhimiza kuhusu Sera ya Viwanda na akiwa kama Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Morogoro ni wajibu wake kuwa karibu na wananchi kuwasaidia kwa kutoa mchango wake .

Hata hivyo, amewataka Wazazi kuwa karibu na Watoto wao ili kuhakikisha wanawalinda watoto dhidi ya ukatili wa kijinsia.

Diwani wa Kata ya Kihonda, Mhe. Hamisi Kilongo, amelipongeza Jukwaa kwa kuandaa shughuli kubwa pamoja na kumpongeza Mhe. Mzeru kwa msaada wake kwa wanawake hao.

Diwani wa Viti Maalum na Katibu wa Madiwani Manispaa ya Morogoro, Mhe. Salma Mbando, amesema Mhe. Mzeru amekuwa mtu wa kujitoa hivyo wakina mama wanakila sababu ya kumpongeza na kutimiza ndoto zao bila kumwangusha kwa masaada alioahidi kutoa.

Kwa upande wa Afisa Maendeleo ya Jamii Kata ya Kihonda, Germina Matotay , amesema Kata hiyo imenufaika na mkopo wa asilimia 10 wa Manispaa ya Morogoro ambapo jumla ya Milioni 88,260,00 zilitolewa katika vikundi 16 kutoka mwaka 2015-2023 na kwa sasa vikundi vyote vinajishughulisha na miradi ya Viwanda vidogovidogo, biashara ndogondogo na kuweka na kukopeshana.

Matotay, amesema Jukwaa linatarajia kuwa na miradi ya uchakataji wa chupa za plastiki, pamoja na utengenezaji wa batiki pamoja na usindikaji mafuta ya alizeti ambapo miradi hiyo itaanza mara baada ya kupata mkopo ambao wanatarajia mwaka 2023 kuanza shughuli zake.

Naye Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Kihonda , Mwamin Daud , amemshukuru Mhe. Mzeru, kwa ahadi yake ya kuchangia ununuzi wa mashine kwa kwa ajili ya kuanzisha kiwanda cha uchakataji ambacho kitasaidia kuwakutanisha wanawake na vijana wakike kujifunza ujuzi wa uchakataji wa chupa ambao utawasaidia katika maisha yao ya kijamii na kiuchumi.

Kauli mbiu ya Siku ya Wanawake Duniani mwaka 2023 " MABADILIKO YA TEKNOLOJIA , CHACHU KATIKA KULETA USAWA WA KIJINSIA".


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa