• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MKURUGENZI MANISPAA MOROGORO AFUNGUA MAFUNZO YA UZINGATIAJI WA KANUNI, SHERIA NA TARATIBU ZA UTUMISHI WA UMMA KWA MAKATIBU MAHSUSI, WAHUDUMU, MAKARANI MASJALA, WALINZI PAMOJA NA MADEREVA

Posted on: November 11th, 2019

MKURUGENZI wa Manipsaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, leo Novemba 11, 2019, amefungua  mafunzo ya uzingatiaji wa kanuni, sheria na taratibu za Utumishi wa Umma kwa Makatibu Mahsusi, Wahudumu, Makarani masjala, Walinzi pamoja na Madereva kwenye ukumbi wa Kilimo Manispaa Morogoro.

Akizungumza na Waandishi wa habari , amesema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo juu ya uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na Taratibu za Utumishi wa Umma.

Amesema kuwa mafunzo hayo yameendeshwa na wawezeshaji kutoka Chuo kikuu Mzumbe , hivyo amewaomba watumishi kuzingatia mafunzo hayo  muhimu kwani yanawajengea uwezo watumishi kimaadili katika kazi  za kila siku.

"Tumewaandalia mafunzo haya ikiwa ni sehemu ya wajibu wangu kama mwajiri wenu wa kuwajengea uwezo ili hatimaye muweze kuongeza ufanisi wa kazi kila mmoja katika eneo lake la kazi, nyinyi ni watu muhimu sana kwenye taasisi yoyote, nawaomba mjiamini vya kutosha ,muwe familia moja na ukipigiwa simu pokea maana muda mwingi tunautumia ofisini,  mungu amekupa ulinzi wake , cheo kikiondoka tayari nuru inaondoka , tujiepushe na majungu ila ukiwa na wazo la kuboresha , ofisi yangu ipo wazi karibuni kwa ajili ya kuijenga Manispaa yetu" Amesema  Sheilla.

Aidha, amekipongeza Chuo Kikuu cha Mzumbe kwa kujitoa kwao katika ushirikiano wa mafunzo hayo pamoja na Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, akisema matarajio yake ni kwamba baada ya mafunzo hayo watumishi wataacha kufanya kazi kwa mazoea na wataenda kuwatumikia wananchi kwa kutoa huduma bora pamoja na kutunza siri za ofisi.

Mbali na mafunzo hayo, amewataka watumishi kujiunga na vikoba kwani mishahara waliyoanyo haiwatoshi katika kuendeleza familia zao.

Amesema vikoba vinasaidia sana , kwani wataongeza vipato na kuweza kuendesha familia kama vile kusomesha watoto pamoja na kuwa na biashara ndogo ndogo zitakazo wawezesha kujikwamua kimaisha.

Naye Afisa Utumishi wa Manispaa ya Morogoro Waziri Kombo, amesema mafunzo hayo yamehudhuriwa na jumla ya watumishi 99, huku akitarajia kila mtumishi mara baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo watumishi wataachana na utendaji kazi wa mazoea.

Amesema  kuwa, wamewalenga hao kwanza kwani wao ndio wasaidizi katika ofisi pamoja na kutunza siri za ofisi, hivyo amewataka wabadilike na kuendana na kasi ya Mhe.Rais Dkt John Magufuli ya kuchapa kazi kwa bidii pamoja na kufuata misingi ya utawala bora.

" Niwaombe watumishi wenzangu, tusifanye kazi kwa mazoea, wengi wetu tunafanya kazi kwa mazoea, sheria , ukiangalia kanuni na sheria pamoja na kimtazamo wa ufanyaji kazi umebadilika, Rais wetu anahitaji matokeo chanya kwa maendeleo ya Taifa,  hivyo lazima tubadilike ili kuendana na kasi yake na asiye badilika tutamchukulia hatua za kisheria " Ameongeza Kombo

Aidha amesema baada ya mafunzo hayo, watakuja kufanya mafunzo kwa wakuu wa idara mbali mbali wa Manispaa ya Morogoro ili nao kuwajengea uwezo wa kuzingatia kanuni, sheria na taratibu za utumishi wa Umma.

Katika hatua nyengine,  Mwenyekiti wa kikao hicho ambaye pia ni msaidizi kumbu kumbu, Bi: Anastazia Mgimba, amemshukuru Mkurugenzi wa Manispaa kwa  kuandaa mafunzo hayo kwani yatawajengea uwezo mkubwa wa kuwatumikia wananchi na kutoa huduma bora ikiwamo kutunza siri za ofisi pamoja na kuzingatia sheria na kanuni  na taratibu za Utumishi wa Umma.

Kwa upande wa William Paul Mollen, ambaye ni Askari wa Jeshi la akiba Manispaa ya Morogoro, amesema wao wameyapokea mafunzo hayo na kuahidi kutoa ushirikiano kwa wakufunzi wa mafunzo kwani yataleta tija kubwa katika utoaji wa huduma bora.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa