• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MKURUGENZI MANISPAA YA MOROGORO AAHIDI USHIRIKIANO JUKWAA LA WANAWAKE MANISPAA YA MOROGORO

Posted on: July 9th, 2020

MKURUGENZI wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, amesema ataendelea kushirikina na Uongozi wa Jukwaa la Wanawake Manispaa ya Morogoro katika kuhakikisha wanasogeza huduma karibu kwa wanavikundi wanaowaongoza.

Kauli hiyo ameitoa leo Julai 09, 2020 Ofisini kwake mara baada ya kutembelewa na Uongozi wa Jukwa hilo na kumpongeza kwa kazi anazozifanya za kuwahudumia wananchi wa Manispaa ya Morogoro pamoja na kusimamia vyema miradi ya Maendeleo.

Lukuba, amesema amefurahishwa saana na ujio wa Uongozi huo wa Jukwaa Ofisini kwake kwani tangia awasili Manispaa ya Morogoro hajawahi kupata ugeni kama huo Ofisini kwake.

'"Nimefurahishwa sana na ujio huu, tangia nifike hapa nilikuwa napata shida sana ya kuwafikia wakina mama kwa karibu lakini kwa ujio wao tunafungua ukurasa mpya , tunaamini hata ile mikopo tunayoitoa kwa Vikundi vyetu hususani wakina Mama Uongozi huu una msaada mkubwa katika usimamizi, endeleeni kupiga kazi, mikopo hii Mhe. Rais Dkt John Pombe Magufuli, ameitoa kwa ajili ya kuwawezesha kiuchumi kujikwamua na maisha na kuondoa umasikini lakini kulifanya Taifa hili kuingia katika uchumi wa Kati ambapo tayari malengo hayo yameshatimia " Amesema Lukuba.

Aidha, amesema kuhusu changamoto zinazowakabili hususani suala la Ofisi, watashirikiana kuona wanapata Ofisi karibu na Mji ili waweze kusogeza huduma karibu kwa jamii na wananchama wao.

"Nimeona kuna suala la Ofisi limejitokeza, lakini nimewaelekeza wakutane na Meneja wa Stendi ya Mabasi Msamvu waone jinsi wanavyoweza kufanikisha ofisi na kuwa mjini tofauti na sasa ipo mbali jambo ambalo linachangia kutowafikia wanachama wao kwa urahisi, wamesema wanachangamoto ya pango lakini nimewaongezea kiasi cha Shilingi 110,000/= ili iwasaidie katika ulipaji wa pango la Ofisi, wamenipatia kanga kama zawadi nawashukuru sana na waomba wakina mama wengine tuendelee kuwaunga mkono wajasiriamali wetu wa ndani ili kunyanyua vipato vyao na kuweza kurudisha fedha za mikopo wanazopatiwa na Halmashauri" Ameongeza Lukuba.

Naye Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Manispaa ya Morogoro, Bi Marry Kachale, amempongeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro kwa kazi zinazofanyika huku wakimuahidi kumpa ushirikianao zaidi katika kuleta maendeleo .

Bi. Kachale, amesema ujio wo katika Ofisi ya Mkurugenzi ni ni pamoja na kujitambulisha kama Jukwaa la Wanawake Manispaa ya Morogoro, kutambulisha kazi zao wanazozifanya, na kumpongeza Mkurugenzi kwa kazi anazozifanya katika usimamizi wa miradi ya maendeleo.

Amesema kwa kutambua umuhimu na majukumu ya Mkurugenzi wataendelea kumpa ushirikiano wa hali ya juu katika kuhakikisha wanasimamia vyema vikundi vya wakina Mama vilivyopewa mikopo ili virudishe kwa wakati.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa