• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MKUU WA WILAYA MOROGORO, AWATAKA WASIMAMIZI WA VITUO VYA UCHAGUZI KUZINGATIA SHERIA , KANUNI , TARATIBU NA MIONGOZO KUFANIKISHA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA AMANI.

Posted on: November 23rd, 2019

MKUU wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Regina Chonjo, amewataka wasimamizi wa Vituo vya Uchaguzi kuhakikisha wanasimamia vyema Sheria, kanuni , taratibu pamoja na miongozo ili uchaguzi uwe wa haki na amani bila ya uvunjifu wowote wa amani.

Hayo ameyasema leo Novemba 23, 2019 , wakati wa ufunguzi wa Semina ya mafunzo kwa Wasimamizi wa Uchaguzi iliyoandaliwa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba.

Amesema kuwa anatambua kwamba maandalizi ya uchaguzi yamepita katika hatua mbali mbali muhimu ambapo kuanzia Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa kutoa Tangazo la uchaguzi Tarehe 28, Septemba 2019.

Aidha, amewakumbusha kwamba bado wasimamizi wa Uchaguzi wana wajibu wa kupitia kanuni za Uchaguzi ya mwaka 2019 pamoja na Mwongozo hususani katika maeneo ya taratibu za upigaji kura (kanuni ya 32-34) upigaji kura (Kanuni ya 35-37) kuhesabu kura na kutangaza matokeo (kanuni ya 38-39) pamoja na mwongozo wa Uchaguzi (ukurasa 13-17).

"  Niwaombe Wasimamizi wa Vituo vya Uchasguzi, maeneo hayo niliyoyataja mkiyasoma kwa umakini mtaweza kufanya na kukamilisha Uchaguzi wetu kwa amani na utulivu, mkatende haki na muhakikishe Walemavu, Wazee, Wagonjwa, Mama Wajawazito pamoja na wanaonyonyesha muwape vipaumbele kwani hili ni kundi muhimu sana lililopewa nafasi yake katika jamii" Amesema DC Chonjo.

Mwisho  ni matarajio yangu kuwa mtaifanya kazi hii mliyopewa kwa uaminifu na uadilifu mkubwa, huku akiwatakia kila la kheri katika uchaguzi huo.

Amesema kuwa, hatua zote alizozitaja kama zitafanyika kwa waledi mkubwa na kwa kuzingatia miongozo ni matumaini yake makubwa kwamba zoezi la upigaji wa kura litakwenda vizuri na kwa waledi wa hali ya juu bila ya kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa Wananchi na wagombea kwa ujumla.

Aidha ameongeza kuwa  Serikali kwa kutambua umuhimu wa Uchaguzi huo, imejipanga vizuri na vifaa vyote muhimu  kwajili ya Uchaguzi vimeshaletwa na kupokelewa, hivyo amempongeza Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa maandalizi mazuri ya Uchaguzi.

"Niwaombe Wasimamizi wa Vituo pamoja na Wasimamizi wasaidizi wa Kata na Mitaa , mnawajibu wa kuhakikisha vifaa vya Uchaguzi vinatunzwa ili baadae vije kutumika kwa Chaguzi nyingine zijazo, unatakiwa kuwa mwaminifu , mchapakazi, muadilifu, mzalendo na mzingatiaji maadili na Utumishi wa Umma" Ameongeza kusema DC Chonjo.

Kwa upande wa Msimamizi wa Uchaguzi Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Ndg. Waziri Kombo, amesema Wasimamizi wa Vituo wana wajibu wa kupanga, kusimamia na kuendesha uchaguzi katika misingi inayowezesha Uchaguzi kuwa huru na haki na kwa kufuata Katiba ya Nchi, Kanuni za Uchaguzi na Sheria nyingine za Nchi.

"Washiriki wa mafunzo haya naomba niwakumbushe mmepewa dhima kubwa sana ya kusimamia jambo ambalo lina maslahi mapana kwa ustawi wa Nchi yetu katika nyanja zote za kiuchumi, kisisasa, kijamii, kiutamaduni na Kidemokrasia fanyeni kazi vizuri tuzidi kulinda amani ya Taifa letu"" Amesema Waziri Kombo.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kuweza kufika na kufungua mafunzo hayo, lakini kubwa zaidi amewataka Wasimamizi wazingatie muda wa kufungua vituo kwa kufuata kanuni na Mwongozo wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Mwaka 2019 na kama walivyoelekezwa katika mafunzo.

Pia amewataka Wasimamizi wasasidizi wa Vituo wahakikishe wanasimamia zoezi la Uchaguzi katika vituo vyao bila kujali jinsia, kabila , Chama na hali yoyote aliyonayo mpiga kura kwa mfano watu wenye ulemavu wa aina yoyote.

Msimamizi Msaidizi kituo cha Geza Ulole Kata ya Kauzeni , Mtendaji wa Mtaa wa Kauzeni, Ahmad Juma Almas, amemshukuru Mkurugenzi wa Manispaa kwa kuanzisha mafunzo hayo kwani yamewakumbusha wajibu wa kufanya kazi na kujenga uaminifu na kujizua na vitendo vya rushwa.

Naye Dorica Uledi,ambaye ni Mwalimu wa Shule ya Sekondari Uluguru, amesema semina hiyo imewasidia kwa upande wa kujua wajibu wao hivyo ameahidi kutoa ushirikiano kuhakikisha zoezi la uchaguzi linakamilka kwa amani.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa