• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MOROGORO KUJENGA HOSPITALI KUBWA YA KISASA YA RUFAA BAADA YA KUPATA EKARI 100

Posted on: November 13th, 2017

SERIKALI ya mkoa wa Morogoro inatarajia kuanza mchakato wa ujenzi wa hospitali kubwa ya rufaa itakayokidhi utoaji wa huduma zote muhimu za wagonjwa baada ya kukabishiwa eneo la ekari 100 kutoka kwa wamiliki wa Dominion Plantation Ltd.

Wamiliki hao pia wametoa ekari nyingine 1,000 kwa ajili ya kujibu matatizo ya wananchi eneo la Tungi , Manispaa ya Morogoro ambao wamejenga makazi ya kudumu ndani ya shamba la mkonge linalomikikiwa kisheria ili waweze kupimiwa viwanja vya makazi .

Mshauri wa mradi wa Star City ,Dan Mrutu alisema hayo hivi wakati wa halfa ya makabidhiano ya ekari 100 zenye thamani ya dola milioni mbili kutoka kwa Dominioni Plantation kupitia Star City kwa Serikali ya mkoa wa Morogoro kwa ajili ya kujenga hospitali kubwa ya Rufaa ya mkoa.

Mrutu , alisema Dominioni Plantation inamiliki ekari 10,661 zilizokuwa zikilimwa zao mkonge ambapo kwa sasa imeanzishwa Kampuni ya Star Infrastucture Development (T), Ltd ambayo inasimamia masuala ya uwekezaji mkoani Morogoro, ( Special Economic Zone).

Alisema , chini ya mradi wa Star City ekari 1,100 zimetolewa kati ya hizo 100 kwa Serikali ya mkoa wa Morogoro kwa ajili ya kujenga hospitali kubwa ya Rufaa na nyingine 1,000 zimetolewa kujibu matatizo ya wananchi ambao wamejenga mkazi ya kudumu ndani ya shamba hilo linalimikikiwa kisheria.

Mshauri wa Mradi huyo alisema, baada ya kutolewa kwa ekari hizo , eneo la ekari 9,561zilizobaki litatumika katika shughuli za uwekezaji mkubwa wa viwanda, mahoteli , Vyuo vya Elimu na majengo ya kati ya kibiashara na ekari 500 kujengwa bandari kavu .

Akipokea ekari hizo kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Morogoro , Dk Kebwe Stephen Kebwe , Katibu Tawala mkoa , Clifford Tandari aliipongeza kampuni hiyo kwa kutoa eneo hilo na kusema kuwa michoro ya hospitali hiyo ipo tayari.

Katibu Tawala wa mkoa huyo alisema , kujengwa kwa Hospitali ya Rufaa ya kisasa ya mkoa itaweza kupanua utoaji wa huduma mbalimbali ambazo zilikuwa haiwezi kutolewa .

Alisema ,miaka miwili iliyopita kulikuwepo na mwekezaji wa nje ambaye alihitaji kujenga Hospital ya kisasa ,lakini kutokana na ukosefu wa eneo alishindwa kufanya hivyo na kwa sasa milango ipo wazi kwa mwekezaji huo kuja kuwekeza .

Naye Meya wa Manispaa ya Morogoro Pascal Kihanga licha ya kuwashukuru wamiliki wa Dominion , aliwataka kuharakisha kufanyika kwa marekebisho ya ramani ya kwa kuziondoa ekari 1,100 ili shughuli za upimaji viwanja na ujenzi wa miradi hiyo mikubwa iwenze kuanza mara moja.

“ Halmashauri haina kikwazo , tayari baraza la madiwani limepitia upimaji wa viwanja eneo hilo na kunachosibiriwa wezetu mrekebishe ramani yenu kwa kuziondoa hizi ekari kutoka ramani ya zamani” alisema Kihanga.

Kwa upande wake Mganga mkuu wa mkoa wa Morogoro , Dk Frank Jaccob alisema kutokana na ukubwa wa eneo hilo ,hospitali ya rufaa ya mkoa itakayojengwa inakidhi mahitaji yote muhimu katika utoaji huduma kwa wagongwa wa aina zote na eneo hilo pia litatumika kujenga vyuo vya utabibu , maabara na madaktari.

Kwa mujibu wa Mganga mkuu wa mkoa , hospitali inayotumika sasa ya rufaa ni majengo yaliyokuwa ni makambi ya askari waliokuwa wamerejea nyumbani baada ya kumalizika kwa vita kuu ya pili mwaka 1945 na yamekuwa wakikarabatiwa mara kwa mara na kuongezwa kutokana na mahitaji.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa