• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

RAIS SAMIA AWATAKA WAFANYAKAZI KUWA WAADILIFU, KUFANYA KAZI KWA WELEDI

Posted on: May 1st, 2023

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka Wafanyakazi wa Sekta zote hapa nchini kufanya kazi kwa Weledi na kuwa waadilifu katika utendaji wao kazini.

Rais Samia ameyasema hayo Mei 1 mwaka 2023, wakati akihutubia Viongozi, Wafanyakazi na Wananchi kwenye kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) ambayo Kitaifa yamefanyika katika Uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro.

Dkt. Samia amesema pamoja na Wafanyakazi hao kudai maslahi yao ya kazi bado wanatakiwa kuwa waadilifu na kufanya kazi kwa weledi katika kutekeleza majukumu yao.

“kwa hiyo pamoja na kudai mishahara bora, lakini uadilifu na weledi kazini ndio utaleta maisha bora kwa wafanyakazi...”. Amesema Rais Samia.

Sambamba na hilo Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewahakikishia wafanyakazi kuwa Serikali itaendelea kuboresha na kuimarisha mazingira ya kazi ikiwemo, kuwapandisha madaraja wafanyakazi, kuwaongezea mishahara na posho za wafanyakazi.

Katika hatua nyingine, Rais Samia amesema kutakuwa na nyongeza za mishahara kwa wafanyakazi ambayo itakuwa inaongezeka kwa kila mwaka, nyongeza hiyo inatarajia kuanza mwaka huu 2023.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa wakati akitoa salam za Mkoa, ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa juhudi kubwa zinazofanywa katika kuwaletea wananchi maendeleo.

Mhe. Fatma Mwassa ameongeza kuwa katika kipindi cha miaka miwili ya uongozi wa Rais Samia wafanyakazi Mkoani Morogoro wameboreshewa maslahi yao ikiwemo kupandishwa madaraja takribani wafanyakazi 7108 wamepandishwa madaraja, 2030 wameajiriwa kwa sasa Mkoa umepata kibali cha kuajiri wafanyakazi 3891 wa kada mbalimbali pamoja na kuongeza mishahara.

Nae Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) Bw. Tumaini Nyamhokya ameishukuru Serikali sikivu ya Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwajali wafanyakazi wake kwa kuwaboreshea mazingira na maslahi yao ya kazi, kulipa2 madai yao, kupandisha vyeo watumishi, pamoja na kuwaongezea mshahara.

Maadhimisho hayo ya Mei Mosi kwa Mwaka huu yanaenda sambamba na kaulimbiu isemayo “Mishahara bora na ajira ni nguzo kwa maendeleo ya wafanyakazi, wakati ni sasa”.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa