• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

RC MALIMA AIPONGEZA MANISPAA YA MOROGORO KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2023

Posted on: June 22nd, 2023


MKUU wa Mkoa wa Morogoro , Mhe. Adam Malima, ameipongeza Manispaa ya Morogoro kwa kupata hati safi kwa kipindi cha miaka nane (8) mfululizo kwenye ukaguzi wa fedha mwaka 2021/2022.

Pongezi hizo amezitoa katika Kikao Maalum cha Baraza la Madiwani la kujadili utekelezaji wa hoja na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) za mwaka wa fedha 2021/2022 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Manispaa juni 22/2023.

Akizungumza katika Mkutano huo, RC Malima, ameitaka Manispaa ya Morogoro kufanyia kazi maoni na mapendekezo yaliyotolewa na mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za Serikali CAG ili kuendelea kupata hati safi.

"Ninampongeza Mkurugenzi na watendaji wote wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa kushirikiana vyema na Baraza la Madiwani kwa utendaji kazi mzuri ulioleta matokeo mazuri na kuiwezesha Halmashauri kupata hati safi kwa kipindi cha miaka nane , lakini niwaombe Madiwani hii Manispaa ni yenu watendaji hawa ni wapita njia tu, tushikamane kuhakikisha tunaboresha huduma za jamii kama Ilani ya CCM inavyotaka chini ya Mwenyekiti wake ambaye ndiye Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan .”Amesema RC Malima.

Vilevile ameitaka Manispaa kusimamia vyanzo vya mapato vilivyopo ndani katika kuongeza mapato ya Halmashauri na sio kutegemea vyanzo vya nje.

Akisoma taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Kwa mwaka wa fedha 2021/2022, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mkoa wa Morogoro, CPA, Peter Mwabwanga, amesema Manispaa ya Ubungo ilikuwa na hoja 68 ambapo kati hizo hoja 58 zilijibiwa vizuri na hoja 10 zimebakia na hoja 6 mpya na hoja 4 za zamani.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Morogoro Mjini, Fikiri Juma, amewataka watendaji na watumishi kuhakikisha kwamba wanawapatia ushirikiano mzuri Madiwani wanapotaka kuongea na wananchi wao katika kutatua kero na changamoto za wananchi.

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Rebeca Nsemwa, ameipongeza Manispaakwa kupata hati safi, hati hiyo imekuja kutokana na ushirikiano baina ya Baraza la Madiwani, Mkurugenzi, Wataalamu , Chama Cha Mapinduzi CCM pamoja Pamoja na watumishi kwa kufanya kazi kwa kujituma na kufuata vigezo na malengo waliyojiwekea.

Kwa upande wa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro na Diwani wa Kata ya Mazimbu , Mhe. Pascal Kihanga, amewataka watendaji kujitahidi kukusanya mapato pamoja na kuweka utaratibu mzuri wa kuweza kushughulikia changamoto za Wananchi.

Mkurugenzi Manispaa ya Morogoro amesema kuwa haya ni mafanikio makubwa sana kwa Manispaa , kwani kitendo cha kupata hati ya ukaguzi inayoridhisha kwa muda wa miaka nane mfululizo imetokana na utendaji kazi mzuri unaooneshwa na watumishi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa