• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

RC SHIGELA ATANGAZA NEEMA KUFUNGULIWA KIWANDA CHA TUMBAKU MOROGORO.

Posted on: June 13th, 2022

MKUU wa Mkoa wa Morogoro,Mhe. M,artine Shigela, amesema kufunguliwa kwa kiwanda cha Tumbaku Mkoa wa Morogoro kitatengeneza mazingira mazuri ya mzunguko wa fedha na kutoa ajira kwa wananchi.

Kauli hiyo ameitoa Juni 10/2022 alipokuwa akitembelea kiwanda hicho ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kutembelea Kata zote za Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro aliyoianza mwanzoni mwa wiki hii kwa ajili ya kutembelea miradi ya maendeleo na kutatua kero za wananchi.

Baada ya kutembelea na kuongea na Uongozi wa kiwanda hicho cha Tumbaku ,RC Shigela, amesema kiwanda hicho kilikuwa kimeajiri watu zaidi ya 3000 na wote walipoteza kazi baada ya kiwanda hicho kusimama.

Aidha, RC Shigela, ameishukuru Serikali ya Awamu ya sita chini ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa ushawishi wake wa kuwashawishi wawekezaji kuwekeza Tanzania.

"Nimefurahi sana kuona shehena ya zao hili kutoka mikoani kuanza kuingia na baadhi ya wafanyakazi kiwandani hapo wakiwa kazini, niendelee kumpongeza Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuifungua nchi na kushawishi wawekezaji kuja kuwekeza hapa nchini lakini pia nampongeza sana mwekezaji mzawa wa kiwanda hiki Ndugu yangu Ahmed Huwel kwa kushawishika kuja kuendesha kiwanda hiki " Amesema RC Shigela.

RC Shigela, ametoa wito kwa wakulima wa zao la tumbaku kuanza kulima kwa wingi zao hilo kwa kuwa sasa wana uhakika wa kupeleka tumbaku yao katika kiwanda hicho ambacho kimeanza kufanya kazi.

“kwa hiyo kuna gap la tani elfu sabini ambazo kama wakulima na wananchi tuhamasike kwenda kuzalisha tumbaku kwa wingi kwa sababu tuna uhakika wa soko” Ameongeza RC Shigela.

Naye Mkurugenzi wa kampuni mpya tumbaku nchini iitwayo Amy Holdings, Ahmed Mansoor Huwel ambaye pia ni mnunuzi wa tumbaku nchini kupitia kampuni yake tanzu ya Mkwawa Leaf na mmiliki mpya wa Kampuni ya Tumbaku, ameishukuru Serikali kwa kuonesha ushirikiano na kumshawishi kuwekeza katika sekta na kutamka rasmi kuwa kiwanda sasa kimerudi nyumbani hivyo amewaomba wananchi kulima tumbaku kwa wingi na kwamba malengo yake kufikisha tani 120,000 ifikapo mwaka 2025 hivyo kutoa ajira ya kutosha kwa wananchi.

"Tumelazimika kukifungua kiwanda cha TTPL kilichopo Morogoro ambacho kilikuwa kimefungwa kwa miaka mitatu, na tumefanya hivyo ili kunusuru wakulima wetu hasa baada ya serikali kutuomba tufanye hivyo," alisema.



Kuhusu utunzaji wa Mazingira, Huwel alisema kampuni yake kwa kuanzia na kwa hali ya dharula, kwa kushirikiana na serikali, Torita na wadau wa tumbaku, itawekeza kwenye tafiti ya udongo kwenye maeneo yote nchini yanayolima tumbaku.



"Tutashirikiana na Torita ili kubaini vionjo halisi vya pembejeo maalum ya tumbaku tofauti ya hali ilivyo sasa, ambapo nchi nzima inatumia aina na idadi ile ile mifuko ya mbolea ya NPK/UREA kwa miaka zaidi ya kumi sasa huku mazingira ya udongo ni tofauti na yanazidi kubadilika," Amesema Huwel.



Aliongeza kuwa kwa pamoja watafanya kazi bega kwa bega na wakulima kupitimia mfumo wa ushirika na Bodi ya Tumbaku ili kusukuma juhudi za serikali za kubadilisha mabani ya zamani ya kukaushia tumbaku yanayotumia nishati ya miti kwa kiwango kikubwa ukilinganisha na mabani ya kisasa.



Alisema kwa kufanya hivyo nchi itaweza kuzalisha tumbaku bora na sio bora tumbaku inayoendana na viwango vya kimataifa yaani compliant crop.



Alisema kampuni yake kwa kuanzia itaajiri wafanyakazi wa kuajiriwa wasiopungua 900 na huku wale wa msimu ambao mara nyingi hufanya kazi viwandani watakuwa kati ya 3000 hadi 5000 kutegemeana na msimu ulivyo.



Kampuni ya kitanzania Amy holdings imenunua mali zote za kampuni ya kimarekani Tanzania Leaf Tobacco Company(TLTC) kikiwemo kiwanda cha tumbaku cha Tanzania Tobacco Processors Limited (TTPL).



Kampuni ya TLTC ilifunga biashara zake hapa nchini miaka mitatu iliyopita na hivyo kuwarejesha majumbani zaidi ya wafanyakazi 600, athari ambayo pia iliwakumba maelfu ya wakulima na familia zao ambao walikosa soko la tumbaku yao huku maelfu ya watu wengine kwenye mnyororo huo wa thamani wa zao hilo wakiathirika.



Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kumteua Mhe. Hussein Bashe kuwa Waziri wa Kilimo kwa kuwa amesema ni kiongozi mahili kiutendaji na mfuatiliaji wa mambo.



Aidha, amemshukuru Waziri Bashe kwa jitihada zake ambazo alianza kuzifanya tangua akiwa Naibu Waziri katika Serikali ya awamu ya tano kwa kuhangaika kukirudisha kiwanda hicho hadi jitihada zake kuzaa matunda akiwa Waziri katika ya Serikali ya awamu ya sita, na kwamba jitihada zake zinakwenda kuwakomboa kiuchumi wananchi zaidi ya 5,000 pamoja na familia zao waliaokuwa wameachishwa kazi wakati kiwanda hicho kimesimama.



Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando ambaye kiwanda hicho kipo katika eneo lake ameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa uongozi wa kiwanda hicho na kwamba hayuko tayari kuona kiwanda hicho kinasimama tena kwa changamoto zozote ambazo zitakuwa ndani ya uwezo wake.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa