• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

SERIKALI ITAENDELEA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAWEKEZAJI NA WAFANYABIASHARA NCHINI-WAZIRI KAIRUKI.

Posted on: December 5th, 2019

SERIKALIya  Awamu ya Tano itaendelea  kutatua changamoto zawawekezaji na wafanyabiashara nchini, kwa kuendelea kushirikiana kwa karibu nawadau mbalimbali kufanya mapitio ya Sera na Sheria ya Uwekezaji kwa lengo lakuboresha mazingira ya kuwekeza na kufanya biashara hapa nchini.

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu ,Uwekezaji  Angellah Kairuki alisema hayo  jana katika hotubayake katika  mkutano wa  Mashauriano kati ya Serikali ,Wafanyabiashara na Wawekezaji mkoani Morogoro uliofanyika mjini hapa.

 

Waziri Kairuki alisema ,jukumu la msingi la Serikalini  kuhakikisha kwamba sekta binafsi inawezeshwa kufanya biashara nakuwekeza katika mazingira ambayo ni wezeshi na yatakayopelekea biashara nauwekezaji wao kuzalisha kwa gharama nafuu na kuuza bidhaa zao kwa bei yaushindani.

 

Alisema , Serikali kupitia Ofisi ya Wazirimkuu  (Uwekezaji) inajiandaa   kuja na Sheria mpyaitakayoitwa Sheria ya Uwezeshaji wa Biashara (Business Facilitation Act) ambayokimsingi ndiyo itafanya utekelezaji wa yote ambayo yameelekezwa katikaBlueprint. 

 

Waziri Kairuki alisema, pia tayari Serikali imechukua hatua zakupunguza utitiri wa kodi, tozo na ada ambazo kwa muda mrefu zilikuwa kero kwawafanyabiashara na wawekezaji.

 

Alisema , kupitia  Bunge la Bajeti la mwaka 2018/2019na 2019/2020 zimefutwa takribani kodi, tozo na ada mbalimbali zipatazo163  na nyingine zilipunguzwa viwango vyake.

 

“ Kufuatia mabadiliko haya  sasa wawekezaji nawafanyabiashara wataweza kuokoa gharama na muda wa kutembelea ofisi mbalimbaliza uthibiti kwa ajili ya kupata vibali.  

 

Waziri huyo alisema , kutokana na mkakati huokutakuwepo  na uzalishaji wenye tija hata ukuaji wa uchumi wa Nchiutaongezeka na hivyo kuongeza fursa za ajira hususani kwa makundi ya wakinamamana vijana. 

 

 

Nao Wafanyabiashara na wawekezaji waliojitokeza katika mkutanowa Mashauriano ulioongozwa na Mawaziri  10 miongoni mwao nane niManaibu Mawaziri kwa nyakati tofauti  wameeleza kuwa kinachowakwamisha katika shughuli zao ni Utitili wa Kodi unaosababishwa na Mfumo usiorafiki kwa taasisi za serikali zilizopewa jukumu la kukusanya Kodi.

 

Mkutano huo wa siku moja ulihudhuriwa na wadau na viongoziwa  ndani na nje ya mkoa wa Morogoro,wakiwemi viongoziwa  serikali wa wizara  mbalimbali na watendaji ngazi zamikoa, wilaya na Halmashauri.

 

Wafanyabiashara hao wanasema pamoja na dhamira ya serikalikutaka kufikia uchumi wa kati kwa uwekezaji wa viwanda, kinacho wakwamishakuendana na sera hiyo ni mfumo wa Kodi unaowafanya kushindwa  hatakufikia  malengo yao.

 

Mwenyekiti wa jumuiya ya wafanyabiashara Tanzania Ally Mambaalisema kumekuwa na changamoto kwa baadhi ya Sheria natozo  zinawakandamiza na kushindwa kujiongeza katika biashara zao.

 

Mambo alisema,pamoja na kufanyika kwa vikao na baadhi yahalmashauri katika Suala la service levy,lengo ni jema la kuhakikisha Serikaliinapata mapato na wafanyabishara wanaendelea kufanya biashara na wamekuwahawatoi maelezo ya kutosha Jambo linalowakatisha tamaa kuendelea kufanyaUwekezaji.

 

Naye Mwakilishi wa wafanyabishara wa Mahoteli Mittah Muriaalisema bado suala la hoteli levy limekuwa likiwakandamiza wakati bado wanalipaVAT na kwamba hiyo Kodi ya namna ya ukokotoaii imekuwa haina maelezo ya kutoshampaka Sasa..

 

"Kodi ya hoteli levy bado si rafiki kwa mfanyabiashara natunaomba iangaliwe,"alisema Muria.

 

Wafanyabiashara wadogo Machinga, wakaomba vitambulisho vya awamuya pili vya Rais pamoja na kuwajari na kuwatambua viwe na picha kwa kilamfanyabiashara.

 

Mwenyekiti wa wafanyabiashara wadogo Faustine France alisema,kumekuwa na changamoto ya wafanyabishara kupeana kitambulisho kutokana nakutokuwa na picha,huku wakaomba kutengewa maeneo ya kudumu yawafanyabiashara,ili waweze kufanya biashara bila tatizo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa