• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WATOTO MIL 8,082,838 KUPATIWA CHANJO YA SURUA NA RUBELLA

Posted on: October 18th, 2019

Watoto wapatao 8,082,838 wenye umri chini ya miezi tisa hadi umri wa miaka mitano wanatarajiwa kupata chanjo ya Surua na Rubella na wengine  millioni 4,041,934 wenye umri wa mwaka mmoja na nusu watapatiwa chanjo ya kuzuia ugonjwa wa kupooza(Polio)

Hayo yamesemwa  Octoba 17 mwaka huu na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Chanjo ya Surua,Rubella na Polio kwa mwaka 2019 iliyofanyika kitaifa mkoani Morogoro.

Aidha,Waziri Ummy Mwalimu amesema ,hivi sasa   Serikali kupitia Wizara hiyo inatoa chanjo  tisa ikiwa ni kinga dhidi ya magonjwa 13 yakiwemo magonjwa ya kifua kikuu,kupooza,kifaduro,donda koo,pepopunda,homa ya ini,Kichomi,uti wa mgongo,mafua makali,kuhara,surua,Rubela na saratani ya mlango wa kizazi.

"Ni dhahiri kuwa haya ni mafanikio makubwa ikilinganishwa na mwaka 1975 tulipokuwa tukitoa chanjo dhidi ya magonjwa matano tu"amesema Waziri Ummy.

Aidha amesema zoezi la kampeni hiyo litagharimu takribani Tsh.Bilioni 11.9 sawa na dola za kimarekani Milioni 4.59 huku lengo kuu likiwa ni kushiriki katika mkakati wa kimataifa katika kutokomeza ugonjwa wa Surua na Rubela ili kuchangia katika kupunguza vifo vya watoto hapa nchini.

Waziri Ummy amesema tayari Tanzania imefanikiwa kufikia lengo la Milenia la kupunguza vifo vya watoto chini ya miaka mitano kutoka vifo 104 kati ya vizazi hai 1000 kwa mwaka 2004/2005 hadi vifo 54 kati ya vizazi hai 1000 mwaka 2013.

Naye mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dk Ketsela Mengistu amesema Shirika hilo litaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kutokomeza magonjwa yanayozuilikakwa chanjo.

Dkt.Ketsela amewataka watanzania kushiriki kikamilifu katika kampeni hizo ili kusaidia kupunguza vifo vya watoto vinavyotokana na magonjwa hayo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro  Mhe.Loata Ole Sanare amesema ,jumla ya watoto 328,462 wanatarajiwa kupata chanjo ya Surua na Rubela huku watoto  136,764 watapatiwa chanjo ya polio mkoa wa Morogoro.

Amesema kampeni hizo hufanyika kila baada ya miaka mitatu ambapo mara ya mwisho ilifanyika mwaka 2014 wakati chanjo ya Rubela ilipoanza kutolewa kwa mara kwanza ambapo ilianza kwa watoto chini ya miaka 15.

Kampeni hii inatarajiwa kufanyika kwa siku tano kuanzia Oktoba 17 hadi Ocktoba 21 itakapohitimishwa.Kauli mbiu ya kampeni ni "Chanjo ni kinga,kwa pamoja tuwa kingine"

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa