• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WAZEE WATAKIWA KUWA NA IAMANI NA SERIKALI

Posted on: October 19th, 2023


Mratibu wa Wazee wa Manispaa ya Morogoro, Bi. Hamisa Kagambo, ameyataka mabaraza ya wazee kuendelea kushirikiana na Serikali na kuwa na imani nayo kwani Serikali ipo pamoja nao katika kuhakikisha inatekeleza afua mbalimbali kwa ajili ya ustawi wa wazee.

“Manispaa ya Morogoro inaendelea na juhudi za kuhakikisha Ustawi wa Wazee unaimarika ikiwemo kuimarisha mifumo ili wazee wapate huduma za kijamii kama Afya, ulinzi, usalama na matunzo kwenye makazi ya wazee” alieleza Kagambo.

Kagambo amesema hayo tarehe 19.10.2023 katika sherehe ya maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani, iliyofanyika katika ukumbi wa Double M- Mazimbu ambapo jumla ya wazee 100 wameweza kupimwa magonjwa mbalimbali ikiwemo kisukari na presha.

Naye Mkurugenzi wa Asasi isiyo ya Kiserikali ya Woman Of Substance, Bi. Mariam Mlembele, ametoa wito kwa wazee kuwaandaa na kuwalea vijana kwa ajili ya maisha ya uzeeni ikiwa ni pamoja na kukemea vitendo vyote vilivyo kinyume na maadili ya kitanzania.

"Katika zama hizi tunahitaji zaidi Wazee waendelee kufanya mengi ili kuambukiza vizazi vipya tabia njema na kuwezesha nao kufikia uzee ulio mwema lakini cha kusikitisha hivi karibuni kumekuwa na Wazee wanaoripotiwa kufanya matukio ya ajabu yasiyolingana na umri wao mfano kubaka na kulawiti watoto, kuwaoza watoto wadogo na kupandikiza imani mbaya" Ameongeza Mlembele.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Kata ya Mazimbu, Isack Wella, amesema kuwa ili wazee wajikwamue kiuchumi katika baraza lao wamepanga kuwa na miradi ya maturubai, viti vya plastiki, na Mahema ambavyo vyote vina gharama ya Shilingi Milioni 1 laki 6.

Wella, amesema Kata ya Mazimbu ina Wazee 700 katika Mitaa yote 7 ambapo kati ya wazee hao, wazee 402 ndio wameweza kupatiwa Bima ya Afya ya Msamaha wa Matibabu.

Nao wazee waliohudhuria katika maadhimisho hayo, wameiomba Serikali kupitia Halmashauri zao itunge sheria ndogondogo ili kudhibiti ukiukwaji wa maadili katika jamii, na wameiomba Serikali katika madhimisho ya mwaka 2024 iongeze huduma ya upimaji macho kwani asilimia kubwa ya wazee wanasumbuliwa na matatizo ya macho.

Akitoa salamu za Baraza la Manispaa la Wazee, Katibu wa Baraza hilo la Manispaa, Dkt.Basil Anga,amelipongeza Baraza la Mazimbu kwa maadhimisho mazuri huku akiwaomba Viongozi wa Mabaraza ya Kata na Mitaa ambao wanachangamoto za Uongozi wajitoe na kupisha Viongozi wengine kuongoza.

Naye Mkurugenzi wa Shirika la kuhudumia Wazee Mkoa wa Morogoro, MOREPEO , Samson Msemembo, amesema MOREPEO ni Shirika ambalo lina shughulika na Changamoto za Wazee Mkoa wa Morogoro pamoja na kuwasemea wazee wote katika ngazi mbalimbali za Mitaa, Wilaya, Mkoa hadi Taifa.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa