• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WAZIRI MABULA AAGIZA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA KUONGEZA NGUVU KATIKA KUKAMILISHA ZOEZI LA URASIMISHAJI

Posted on: February 22nd, 2023

WAZIRI wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula, ameziagiza mamlaka za Kupanga, Kupima na Kumilikisha ardhi nchini kuhakikisha zinaongeza nguvu katika kukamilisha zoezi la urasimishaji wa makazi kabla ya kumalizika kwa mwaka 2023 ambao ndio mwisho wa zoezi hilo.

Waziri Mabula amesema hayo leo Februari 22/2023 katika kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa mpango kabambe wa urasimishaji makazi kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi Kuu ya Manispaa ya Morogoro.

Akizungumza katika kikao hicho, Waziri Mabula, amesema kuwa Mamlaka za Serikali za Mitaa inayo jukumu la urasimishaji na upangaji wa miji kwa kushirikiana na Makampuni ya urasimishaji badala ya kuitegemea Wizara kutenga fedha hizo.

" Tumeweka mpango kabambe wa urasimishaji , mwisho mwaka huu 2023, niombe mamlaka za upimaji , usimamizi na uratibu wa ardhi mfanye kazi zenu ipasavyo, niombe mkasimamie vizuri upangaji wa miji ili kuepusha migogoro ya ardhi na kupanga miji vizuri, niwapongeze Manispaa ya Morogoro kwa kufika asilimia 53 ya urasimishaji katika Mkoa wa Morogoro " Amesema Waziri Mabula.

Katika hatua nyengine, amesema maeneo ambayo hayajaendelezwa yanachafua taswira ya Miji na yanapoteza mapato ambayo kama yangeendelezwa yangekuwa na faida kiuchumi, hivyo Viongozi wawaelimishe wananchi kuhusu mipaka ya ardhi pamoja na kuyaendeleza maeneo yao.

Miongoni mwa maagizo aliyotoa kwa Halmashauri nchini ni Halmashauri kukaa na Makapuni waliyoyapa tenda ya kazi ya urasimishaji kukaa nayo ili kuona namna gani gani kazi ambazo hawajakamilisha wanazikamilisha kikamilifu, Kampuni zitakazoshindwa kutekeleza zoezi hilo la urasimishaji wawafutie tenda na kudai fedha zao pamoja na kutokutoa tenda mpya kwa makampuni ambayo hayakumaliza kazi ya urasimishaji.

Dkt. Mabura, amesema , zipo hatua ambazo Wizara ya ardhi imezichukua ikiwemo Wizara kufanya kikao kazi na TAMISEMI kuona namna gani ya kushirikisha Halmashauri kutenga fedha katika Sekta ya ardhi juu ya upangaji na urasimishaji pamoja na kufanya kikao na Makampuni ya urasimishaji ili kuwapa mpango kazi wa utekelezaji wa zoezi la urasmishaji.

Hata hivyo, amesema zipo changamoto ambazo zimejitokeza katika kutofanya vizuri katika mpango kabambe ikiwemo kazi za urasimishaji kuchelewa au kutokukamilika, uchangiaji hafifu wa uchangiaji katika urasimishaji, usimamizi usiolizika kwa mamlaka ya urasimishaji , baadhi ya Makampuni kuchukua pesa bila kumaliza kazi na kutokuwepo kwa kumbukumbu na nyaraka za mapato ya ukusanyaji wa fedha za urasimishaji.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Maendeleo ya Makazi, Wizara ya ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Deogratias Desderius , amesema asilimia 35 ya wananchi Tanzania wanaishi Mjini huku akisema ongezeko la watu ni asilimia 3.2 .

Amezitaka Mamlaka za Serikali za Mitaa kuongeza nguvu katika upangaji wa maeneo , kwani hali inaonesha zaidi ya miji 4310 imekuwa ikichipuka na kukuwa kutokana na Serikali kuboresha huduma za kijamii Vijijini na Mijini.

Amesema kuwa katika kuona zoezi la urasimishaji linafanikiwa , Wizara imeandaa muongozo wa uendelezaji wa nyumba Vijijini na Makazi bora.

Naye Afisa Mipango Miji Manispaa ya Morogoro, Emeline Kihunrwa, akiwasilisha mpango kabambe wa urasimishaji, amesema asilimia 65 limepimwa na asilimia 35 ya eneo lililopimwa bado barabara zake hazijafunguliwa.

Kihunrwa, ametaja mapendekezo ya mpango kabambe wa Halamshauri , miongoni mwa mapendekezo hayo ni kuanzisha vituo vya biashara nje ya mji, urasimishaji makazi holela, utunzaji wa vyanzo vya maji, uendelezaji wa mji, kuboresha mifumo ya maji taka na taka ngumu pamoja na kutenge maeneo ya maegesho.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa