• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WAZIRI MKUU MSTAAFU PINDA ATOA NENO KUHUSU UTAPIAMLO.

Posted on: August 5th, 2022

WAZIRI mkuu mstaafu, Mizengo Pinda amesema suala la utapiamlo linatakiwa kuendelea kupigiwa kelele kwani bado ni kubwa hapa nchini na kusababisha udumavu kwa kiwango cha asilimia 31 kwa watu wake.

Pinda alisema hayo jana wakati wa ufunguzi wa maonyesho ya Nanenane kanda ya mashariki yanayoshirikisha mikoa ya Pwani, Dar es salaam, Tanga na Morogoro yanayoendelea viwanja vya Julius Nyerere.

Alisema suala la lishe bora ni vyema likapigiwa kelele na kuacha kubebeshwa lawama serikali kutokana na watoto wanaozaliwa nyakati nyingine kuwa na uzito mdogo.

Pinda alisema ya kwamba wataalamu wamekuwa wakieleza akinamama wajawazito wengi wamekuwa na upungufu wa damu na wanapofikia muda wa kujifungua na wanapata matatizo na hiyo kutokana na kula vyakula bila kujali lishe bora.

“Mimi natoka Katavi tunatamba kwa kulima mahindi lakini ugali wa mahindi niliozoea ni kwamba ukibolewa ulowekwe kwenye maji wiki moja halafu uanikwe kidogo na kupelekwa kusagwa mashine eti kupata ugali mzuri wa kunukia hii si hoja,”alisema Pinda

Alisema “Kumekuwa na mazoea kuwa wanaokula dona ni wafungwa pekee na hii si sawa pale watu wengi wanakula wanga (stach) ndani yake hakuna kitu sasa tuna mtihani mkubwa wa kusemea lishe,”alisisitiza Pinda

Alisema pamoja na mikoa ya Rukwa na Katavi kuongoza katika kulima zao la mahindi lakini mkoa hiyo ni miongoni mwa inayoongoza katika suala zima la utapiamlo.

Waziri mkuu Mstaafu alisema , wataalamu wamekuwa wakieleza kuwa ili kokomesha suala la utapiamlo ni lazima watu watumie mbogamboga ambacho ni chakula muhimu na kwamba ulimwengu unakili kuwa mboga zenye asili ya Afrika zimekuwa zikiongoza kwa lishe.

“Nataka tutoke hapa kwenda kulima bustani za mboga na sio kulima kwa ajili Biashara pekee bali kulima kwa kula ilikuweza kupata afya bora, hivyo nanenane kwangu tutumie kujifunza kilimo hicho,”alisema Pinda

Hivyo aliwataka wananchi kutumia ufugaji bora huku akiridhishwa na ufugaji bora hasa wa Samaki kwa kutumia njia za kisasa.

Pamoja na hayo alisema sekta ya kilimo bado ni muhimili kwa nchi hivyo kilimo kikiteteleka ni sawa na mtu akiteteleka na mgongo wake hivyo kilimo ni muhimu katika kuleta maendeleo.

Naye Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki kabla ya kumkaribisha Waziri mkuu Mstaafu Pinda, alisema katika kuondoa ukiritimba unaojitokeza ,wizara imeanzisha mfumo wa mazao ya Uvuvi, mifugo na mazao mengine (MIMIS) utakao wawezesha wadau wa mifugo wa zao ya uvuvi kufanya shughuli zao za kupata vibari na mambo mengine kwa haraka na urahisi.

Alisema wizara inaendelea kufanya mabadiliko katika mifumo mbalimbali ya kuoa urasimu na kuwataka wananchi kuondoka kwenye mifumo ya zamani , wizra inaendelea kuhamasisha wafugaji na wananchi kwa ujumla kuhusiana na chanjo mbalimbali za mifugo na sasa aina saba za chanjo zinazalishwa na kiwanda cha serikali.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Morogoro,Fatma Mwasa alisema kuwa mikoa inayounda Kanda hiyo imejipanga kuboresha maonesho ya Nanenane ili kuwezesha wananchi wajifunze teknolojia ya kilimo, mifugo na Uvuvi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa