• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WAZIRI NCHEMBA ATOA ONYO KWA WATENDAJI KUTOTOZA WANANCHI FEDHA KATIKA ZOEZI LA USAJILI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA

Posted on: February 13th, 2018

WAZIRI wa Mambo ya ndani ya nchi Dk Mwigulu Nchemba,amewaonya watendaji wa mitaa na kata ambao wanawatoza fedha wananchi katika zoezi la usajili na utambuzi wa watu linalofanywa na mamlaka ya vitambulisho vya Taifa (NIDA) kuacha mara moja na wale watakaobainika watafukuzwa kazi.

Waziri Dk Nchemba alitoa agizo hilo baada ya kuzindua zoezi la usajili na utambuzi wa watu mkoani Morogoro linalofanywa na Nida na kuwagiza viongozi wa mkoa wa Morogoro kusimamia kwa karibu zoezi hilo na kuwabaini mara moja watendaji wanaowatoza wananchi fedha .

Alisema kuwa Serikali imegharamia kila kitu katika zoezi hilo na hakuna mwananchi anayepaswa kutozwa kiasi chochote cha fedha na kutaka kila mwananchi kujitokeza kujisajili ili kupata vitambulisho hivyo na kuwasisitizia viongozi hao kuhakikisha hakuna mtu ambaye si raia anayepenya na kupewa kitambulisho cha taifa.

Waziri Nchemba aliwahakikishia wananchi wa mkoa  kuwa wizara imejipanga kwa kuhakikisha kwamba ifikapo Desemba 2018 wananchi wote hapa nchini wenye umri wa miaka 18 na kuendelea wawe wameshasajiliwa na kupata namba za utambulisho.

Alisema kuwa dhamira ya Serikali katika zoezi hilo ni kuhakikisha  wananchi wanatumia vitambulisho vya Taifa kwa matumizi mbalimbali na kusisitiza kwamba vitambulisho hivyo vinatolewa bure.

Awali Akisoma taarifa ya utendaji kazi wa mamalaka hiyo ya vitambulisho vya Taifa (Nida) Kaimu mkurugezi mkuu wa Nida Andrew Massawe alisema kuwa tayari vifaa zikiwemo mashine 200 zimesambazwa ili kukidhi mahitaji ya usajili na kuhakikisha ifikapo Aprili 30 mwaka huu zoezi ile liwe limekamilika.

Kaimu mkurugenzi huyo alisema kuwa Nida imetoa ajira za muda mfupi kwa wananchi 200 na kufungua ofisi kwenye wilaya zote ambapo jumla ya maafisa 23 wa kudumu kutoka Nida wamegawanywa kwenye wilaya zote kwa lengo la kusaidiana na watendaji wa wengine kuhakikisha zoezi linafanikiwa.

Massawe alieleza baadhi ya faida za kuwa na kitambulisho cha taifa kuwa ni pamoja na kuweza kupata huduma kirahisi za afya, elimu na fedha na za kiulinzi na usalama.

Katika hatua nyingine Kaimu mkurugenzi huyo aliitaja mikoa ambayo imefanya vizuri katika zoezi hilo la usajili na utambuzi kuwa ni pamoja na Iringa, Mara, Simiyu,Arusha, Geita, Mwanza, Ruvuma, Kilimanjaro na Lindi ambapo alisema kuwa mafanikio hayo yalitokana na uongozi madhubuti wa mikoa hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa mkuu wa mkoa wa Morogoro Dk Stephen Kebwe alisema kuwa jumla ya wananchi 961,309 wenye umri wa miaka 18 na kuendelea watasajiliwa hata hivyo alisema kuwa katika kipindi hiki cha kilimo kinaweza kuwa changamoto kwa wananchi kujitokeza kwani wengi wako mashambani.

Dk Kebwe aliwataka viongozi wa dini kutumia nyumba za ibada kuhamasisha wananchi kujitokeza kwenye zoezi hilo huku akitoa onyo kwa baadhi ya wanasiasa kutopotosha na kubeza dhamira ya zoezi na kwamba yeyote atakayebainika kukwamisha zoezi hilo atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa