• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MAAFISA ARDHI WATAKAOBAINIKA NI VYANZO VYA MIGOGORO YA ARDHI TUTAWAFIKISHA MAHAKAMANI-DKT.NDUMBARO.

Posted on: May 5th, 2025

Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amesema wakati awamu ya kwanza ya Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia kwa Tanzania Bara inakwenda kukamilishwa mwezi Juni katika mkoa wa Dar-Es- Salaam kwenye uwanja wa Mkapa, awamu ya pili ya kampeni hiyo itaweka mkazo kwenye utatuzi wa migogoro ya ardhi kwa kuwa suala hilo limebainika kuwa ni uhitaji mkubwa kwa wananchi, na afisa ardhi yeyote atakaye bainika kuwa chanzo cha mgogoro wa ardhi p pote atachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kufikishwa mahakamani.

"Katika ulimwengu huu wa teknolojia hatutegemei kuwepo na migogoro ya double allocation ya ardhi kwa kuwa shughuli zote zinafanyika kwenye mifumo, hivyo basi afisa ardhi anayesababisha migogoro kwa sababu ya kufanya double allocation, ni lazima tumchukulie hatua kali za kisheria ili kukomesha kabisa tatizo hili. Kufanya double allocation ya ardhi ni rushwa na ni lazima tupambane kuikomesha" alieleza Mhe. Ndumbaro.

Amesema awamu ya pili ya kampeni itafanyika kwenye maeneo yote ya awamu ya kwanza ili kubaini changamoto zilizokuwa zimesalia na kuzitatua zote kwa kuwa wizara itahakikisha miongoni mwa wanatimu wa kampeni ya awamu ya pili kunakuwa na mahakama tembezi (mobile court).

Aidha, Mhe. Ndumbaro amempongeza na kumshukuru Rais Dkt. Samia kwa kuanzisha Kampeni hiyo ambayo imekuwa na manufaa sana kwa wananchi hasa wa maeneo ya pembezoni mwa nchi ambao mara nyingi hulazimika kusafiri  umbali mrefu kufata huduma za msaada wa kisheria.

Amesema kampeni hiyo imekuwa mfano wa kuigwa kote ulimwenguni na imelifanya Taifa la Tanzania kuwa tajika ulimwenguni kote kwa kuwa ndio Taifa anzilishi la kampeni hiyo.

Mhe. Ndumbaro amesema hayo alipokuwa akizungumza na Kamati Kuu ya Nanenane Kand ya Mashariki katika mkutano wa kamati hiyo uliofanyika tarehe 05.05.2025 kwenye uwanja wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, maarufu kama uwanja wa nanenane mjini Morogoro.

Mkutano huo uliongozwa na mkuu wa mkowa wa Tanga, Mhe. Balozi Batilda Burhan na kuhudhuriwa na wakuu wa mikoa ya Tanga, Pwani, Dar-es-salaam na Morogoro, wakuu wa wilaya za mikoa hiyo, wakurugenzi, wataalamu wa sekta husika.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • BALOZI BATILDA ATAKA MAONI YA WADAU KUFANYIWA KAZI KUELEKEA MAONESHO YA NANENANE KANDA YA MSHARIKI 2025

    May 06, 2025
  • MAAFISA ARDHI WATAKAOBAINIKA NI VYANZO VYA MIGOGORO YA ARDHI TUTAWAFIKISHA MAHAKAMANI-DKT.NDUMBARO.

    May 05, 2025
  • WAAJIRI SEKTA BINAFSI RUHUSUNI WATUMISHI WENU KUJIUNGA NA CHAMA CHA WAFANYAKAZI - RC MALIMA.

    May 01, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa