• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

ASILIMIA 90 YA WATU WA MKOA WA MOROGORO WAMESAJILIWA NIDA.

Posted on: November 12th, 2019


MAMLAKA ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) mkoa wa Morogoro imeeleza kuwa, hadi sasa asilimia 90 ya wakazi wa mkoa huo wamesajiliwa na kupata namba za vitambulisho ambazo zinawawezesha pia kusajili line za simu zao kwa njia ya alama za vidole.

Ofisa wa Nida wa mkoa huo ,James Malimo alisema hayo alipokuwa akijibu kero juu ya ucheleweshaji upatikanaji wa vitambulisho vya taifa ambacho pia kwa sasa kinatumika kusajilia line za simu kwa njia ya alama za vidole .

Malimo alisema hayo Novemba 7, 2019 baada ya kutakiwa na mkuu wa wilaya ya Morogoro, Regina Chonjo kwenye mkutano wake aliouitisha kukutana na wananchi wa wilaya hiyo kila mwezi akianzia na Manispaa ya Morogoro kwa ajili ya kusikiliza na kutatua kero mbalimbali ikiwemo migogoro ya ardhi.

Malimo alisema akijibu swali la msingi lililoulizwa na mkazi wa Kola A , Samson Msemembo ambaye alitaka kujua hatua mbalimbali za zoezi la utoaji wa vitambulisho vya Taifa unaoendela kufanyika .

Mkazi huyo alisema , licha ya zoezo hilo kuendelea lakini bado watu wengi hawajaandikishwa na muda wa kufikia ukomo wa kusajili line za simu kwa njia ya alama za vidole wa Desemba 31, mwaka huu unakaribia na watafanyeje iwapo hawatapata kitambulisho hicho baada ya muda huo.

Malimo alisema , Nida ilianza kusajili wananchi kupata kitambulisho cha taifa muda mrefu , lakini baada ya tangazo la Serikali la kusajili upya namba za simu kwa njia ya alama za vidole na kutumia kitambulisho cha taifa , idadi kubwa ya wananchi wanajitokeza ili kutaka kujisajili na kupata kitambulisho cha taifa.

Alisema , baada ya kuona changamoto ya watu kuwa ni wengi na hawajasailiwa , Nida mkoa wa Morogoro iliamua kurudisha mashine za usajili ngazi za kata kuanzia Machi mwaka huu ili kuongea kasi ya uandikishaji na ujazaji wa fomu za Nida.

“ Mpango huu umeleta mafanikio kwani hadi sasa asilimia 90 ya wakazi wa mkoa wa Morogoro wameshasajiliwa na namba za vitambulisho vimezalishwa na zimewasaidia watu kuweza kusajili line zao kwa njia ya alama za vidole kupitia namba ya Nida waliopata “ alisema Malimo.

Hata hivyo alisema ,katika Manispaa ya Morogoro yenye kata 29 ,ni kata moja pekee ya Mji Mpya viongozi wake hawajafika kuchukua orodha ya namba za vitambulisho na kuhimiza kufanya hivyo.

Pia alisema , Nida mkoa wa Morogoro imeongeza muda wa kufanya kazi hadi saa 11 jioni siku za kazi badala ya kutoka saa uliopangwa wa saa 9: 30 alasiri na kwa siku ya jumamosi utoaji wa huduma kwa wananchi itandelea kufanyika kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa 7 : 30 mchana.

Hata hivyo alitumia fursa hiyo kuwataka watendaji wa mitaa na kata za Manispaa ya Morogoro kuwandaa utaratibu utakaowezesha kuwafikia wazee katika ngazi ya kata ili waweze kuhudumiwa kupatiwa vitambulisho vya taifa .

“ Ninachowaomba watendaji wa mitaa na kata ili kuweza kuwafikia wazee maeneo hayo na makundi mengine watuandalie utaratibu maalumu wa kuwahudumia “ alisema Malimo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa