• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC CHONJO ASAMBAZA NDOO 100 ZA KUNAWIA MAJI MANISPAA YA MOROGORO KATIKA KUJIKINGA NA UGONJWA WA CORONA

Posted on: March 28th, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Regina Chonjo,amekabidhi jumla ya Ndoo 100 za kuwekea maji tiririka pamoja na sabuni ikiwa ni jitihada za kujikinga na Ugonjwa wa CORONA Manispaa ya Morogoro.

Akizungumza na Waandishi wa habari, amesema kuwa ndoo hizo zimenunuliwa chini ya ufadhili wa Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini,Mhe. Abdulaziz Abood katika kuhakikisha Wananchi wa Jimbo lake wanajikinga na Ugonjwa wa CORONA.


Amesema kuwa ni jukumu la Wananchi kuzitunza ndoo hizo ili ziendelee kutumika katika maeneo yao ya biashara.


Aidha, amesema Ndoo hizo sio mali ya mtu binafsi bali kila mtu atakuwa na haki ya kuitumia ili kuweza kusaidia katika kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya CORONA COVID -19.


“Leo tunagawa Ndoo hizi katika maeneo tofauti tofauti, kikubwa niwaombe Wananchi kwamba wawe wastaarabu katika kuvitunza isitokee mtu akakichukua akajifanya ni ya kwake, Mhe. Wenu Abood anawapenda sana , katika kuona janga hili linakuwa halina madhara ameona ni vyema akaungana na Wananchi wake kuwasidia ili katotumia ile pesa ambayo ni mitaji yenu msiitumie badala yake ametoa ndoo hizi na sabuni, kikubwa elimu iendelee kutolewa na sisi wenyewe tuwe mabalozi wazuri wa kuelimishana juu ya kujikinga na Ugonjwa huu ambao ni hatari sana ukiangalia Mataifa ya wenzetu wanateketea sana hivyo lazima na sisi tuchukue tahadhari kubwa ya kujikinga ili tuwe salama”Amesema DC Chonjo.


Kwa upande wa Mwananchi, Juma Abdallah, amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Morogoro pamoja na Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini, Mhe. Abdulaziz Abood kwa kuwapatia ndoo na sabuni.


“Tunawashukuru sana Viongozi wetu kwa kuonesha moyo wa kutujali sisi katika vijiwe vyetu tumekuwa tukipeana sana elimu lakini ujio wako tena kwa kutupatia vifaa kama hivi umetufariji sana, sasa tunaungana na Serikali yetu kupaza sauti kwa pamoja ili kuhakikisha kila mwananchi anajikinga na ugonjwa huu na kufanya Taifa letu kuwa salama hususani katika Manispaa yetu ya Morogoro” Amesema Juma.

Pia amechukua nafasi ya Kupongeza Jitihada zinazofanywa na Uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro chini ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Sheila Lukuba pamoja na Mganga Mkuu wa Manispaa ya Morogoro , Dr Ikaji Rashid na timu nzima ya Wataalamu wa Afya kuanzia Ngazi ya Wilaya, Manispaa na Kata hadi kwenye Mitaa kwa jitihada kubwa za kutoa elimu dhidi ya kujikinga na Ugonjwa wa CORONA.

Miongoni mwa maeneo ambayo ndoo hizo zilisambazwa ni pamoja na Stendi ya Daladala Mjini, Stendi ya Bajaji (Jumata) na Wauza Matunda, Soko la Manzese na Vijiwe vya Bodaboda, Soko la Fire Kiwanja cha Ndege, Masika, Stendi ya Daladala Kaloleni, Stendi ya Mabasi Msamvu na maegesho ya Magari ya kukodishwa nje ya Stendi ya Msamvu, Kihonda viwandani, Mazimbu Road, Kihonda kwa Chambo, Barabara ya Ipo Ipo, Soko la Mazimbu jirani na Ofisi ya Kata ya Mazimbu, Chamwino pamoja na Soko la Chamwino.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa