• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC MSANDO AWATAKA WADAU NA WAJUMBE WA KAMATI ZA USHAURI KUISHAURI SERIKALI KUFANIKISHA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: October 6th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Albert Msando, amewaomba wadau mbalimbali wa maendeo kuendelea kuishauri Serikali katika kufanikisha miradi ya Maendeleo.

Hayo ameyasema , Oktoba 06/2021 katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Morogoro (DCC) kilichofanyika Katika Ukumbi wa Mikutano wa Kilakala Soko Kuu la Chifu Kingalu Morogoro .

Akizungumza wakati wa kuongoza kikao hicho, DC Msando, ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya ushauri (DCC) amewataka wadau pamoja na wajumbe wote wa kamati ya Ushauri Wilaya kuendelea kuishauri serikali namna gani ya kuboresha utendaji wa kazi na kuleta maendeleo.

"Ninawaomba wajumbe wote wa kamati hii kuishauri serikali bila kuogopa kwani ushauri wenu ni tija kwa maendeleo ya wilaya yetu" Amesema Msando.

DC Msando, amesema kuwa lengo la kamati ya ushauri Wilaya ni kuhakikisha Wilaya na Halmashauri zinasonga mbele, hivyo wajumbe wasichoke na wawe huru kutoa mapendekezo yao kwa kuchangia mambo mbali mbali kwa mustakabali wa maendeleo ya Wilaya.

"Lengo la kamati ya ushauri ni kuishauri serikali , sisi tupo tukiwa Viongozi wa Wilaya tukisimamia Maendeleo, ili kuhakikisha Wilaya yetu na Halmashauri zetu zinasonga mbele kimaendeleo, siyo kwamba yote tunayoyafanya ni sahihi, na ndio maana lengo la kikao ni kutushauri namna gani ya kuboresha utendaji wetu ili kuleta maendeleo makubwa katika Wilaya na Halmashauri zetu " Amesema DC Msando.

Naye aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mstaafu , Mzee . Steven Mashishanga, ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa kusimamia vyema mapendekezo ya kamati ya ushauri.

" Wajumbe wanafanya kazi nzuri sana, lakini ni vyema katika vikao vijavyo vya kamati kila idara ikaonesha takwimu halisi katika taarifa zake zikiwamo changamoto , idadi ya upungufu wa watumishi ili kamati iweze kutoa ushauri" Amesema Mzee Mashishanga.

Kwa upande wa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoroo, Mhe. Pascal Kihanga, amewataka Wajumbe wa kamati ya ushauri kuzungumzia changamoto na kutoa ushauri kwa uhuru ili yatokanayo yaweze kufanyiwa kazi.

"Pongezi kwa watendaji wote kwa kushirikiana kwa pamoja, hayo yote tunayoyafanya ni kutokana na ushauri wenu, na leo pia Ushauri wenu tumeupokea na tutaufanyia kazi kama tunavyochukua siku zingine, Na kama mnaona jambo haliendi sawa ni ruksa kwenu kutoa ushauri kwa uhuru kabisa na sisi tutaupokea" Mhe, Kihanga.

Naye Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini, Mhe. Abdulazizi Abood, amesema atahakikisha kwamba yale maendeleo yanayotakiwa kufanywa yatafanyika kwa kuongeza msukumo Bungeni katika kuona miradi yote ambayo iempendekezwa inapitishwa.

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Morogoro, Dr. Christine Ishengoma, amesema katika kufikia malengo lazima kuwe na maoni ya watu mbalimbali .

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa