• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DIWANI CHOMOKA KUJA NA MKAKATI WA KUVISAIDIA VIKUNDI KUPATA MASOKO.

Posted on: March 6th, 2023

DIWANI wa Kata ya Mkundi, Mh. Seif Chomoka, amesema ili bidhaa ziweze kuuzika ni lazima wajasiriamali wajikite katika kujitangaza na kutafuta masoko.

Kauli hiyo ameitoa Machi 04/2023 akizungumza na Vikundi vya Wajasiriamali vilivyojitokeza katika sherehe za maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Kata ya Mkundi.

Akizungumza juu ya kuwakomboa wajasiriamali wa Kata hiyo, Mhe. Chomoka amesema ataandaa maonesho ya vikundi vyote vya wajasiriamali kwa kushirikiana na Uongozi wa Chama Cha Mapinduzi Kata pamoja na Uongozi wa Ofisi ya Kata na Uongozi wa Jukwaa ili kuweza kutoa fursa kwa wajasiriamali kujitangaza.

Amesema katika kufanikisha hilo, ataomba ushirikiano kwa viongozi mbalimbali wa Manispaa kuhudhuria katika maonesho hayo ikiwemo na wadau wengine kwa ajili ya kuwatambulisha wajasiriamali wake na kuweza kupata masoko.

" Maonesho haya kwa mara ya kwanza nitagharamia mimi kwa fedha zangu kila kitu, lengo kujitangaza, shauku yangu ni kuona wanawake wa Mkundi wananyanyuka kwa nguvu, nataka kufanya kazi na wanawake wa Mkundi, nitahakikisha kuwa malengo yangu yanafanikiwa kwani nilishatoa mkopo wa milioni 5 ili vikundi vikopeshane , huu ndio mkakati wangu " Amesema Mhe. Chomoka.

Aidha Chomoka, amesema kuwa maonesho hayo yatakuwa yakifanyika kila baada ya miezi 3 na imani yake baada ya kufanyika na kufanikiwa basi wajasiriamali wataweza kugharamia kiasi cha fedha kidogo kuendesha maonesho hayo kwa vipindi vijavyo.

Katika hatua nyengine, ametoa fursa kwa wajasiriamali wa sabuni kuwa kwa sasa masoko yao yatakuwa katika Taasisi zake anazoziendesha ikiwemo Chuo cha St. Joseph, MSJ pamoja na Shule ya A-Plas.

"Nimetangaza fursa kwa wajasiriamali wanaotengeneza sabuni, kuanzia leo, nataka nikutane nao Ofisi kwangu tukubaliane kufanya biashara kupitia Taasisi zangu ninazoendesha, hawa ninawapa masoko moja kwa moja nataka wanawake wa mkundi wajikomboe na hii ndio dhana ya Uongozi ya kuwatumikia na kuwanufaisha wale unaowaongoza" Ameongeza Mhe. Chomoka.

Naye Katibu wa Jukwaa la Wanawake Manispaa ya Morogoro, Clara Kapungu, amewataka Viongozi wa Jukwaaa kutumia fursa zilizopo katika kuvikwamua kiuchumi vikundi vyao.

Kwa upande wa Katibu aliyemaliza muda wake , Paulina Mbawala, amempongeza Mhe. Diwani kwa kuwajali wanawake wa Kata ya Mkundi huku akimuahidi kutoa ushirikiano mkubwa katika kutimiza ndoto zake za kuwasadia wanawake wa Kata hiyo.

Katika maadhimisho hayo, Vikundi vya wajasiriamali vilipata nafasi yha kuonesha bidhaa zao ambazo wamekuwa wakizizalisha.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa