• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

JUMUIYA YA WAAHMADIYYA TANZANIA YAWEZESHA MAJI KWA WAKAZI WA KIHONDA MOROGORO

Posted on: March 5th, 2018

WANANCHI wa mitaa ya Kata ya Kihonda Maghorofani , Manispaa ya Morogoro wameondokana na adha ya kutopata uhakika maji safi na salama baada kujengwa kituo cha kuchota maji ya bomba kupitia ufadhili wa Jumuiya ya Waislamu Waahamadiyya chini ya mradi wake wa Taasisi ya International Association of Ahmadi Architects and Engineers (I.A.A.A.E).

Mkuu wa Chuo cha Ahmadiyya Muslim Jama’at Tanzania, Sheikh Abid Mahmood Bhatti alisema hayo kabla ya kukaribishwa mkuu wa mkoa wa Morogoro, Dk Kebwe Stephen Kebwe , kuzindua mradi wa maji uliojulikana kwa jina la ‘ Water For Life’ katika kituo cha Jumuiya ya Waislamu Waahmadiyya Morogoro na jirani zake .

Alisema , Jumuiya hiyo pamoja na kuwa ni taasisi ya kidini , inayo mipango mbalimbali ya kutoa huduma za kijamii zikiwemo katika sekta ya afya, elimu , umeme na maji.

“ Mradi huu ulianzishwa mwaka jana baada ya kupitishwa na Hadharat Khalifa tul Masih kiongozi mkuu wa Jumuiya ya waislamu waahmadiyya duniani kupitia taasisi ya IAAAE” alisema Bhatti.

Mkuu wa Chuo alisema , jamii ya Kihonda Maghorofani iliyopo karibu na taasisi hiyo wanaweza kuchota maji lita zisizopungua 10,000 kwa siku kwa ajili ya matumizi ya nyumbani .

“ Hapa napenda kuwaomba wananchi kwamba huduma hiii ya kijamii isitumike kwa ajili ya biashara , huduma hii itatolewa bure kwa wakazi wote , bila ubaguzi wa kiitikadi wa kidini na kutolewa kuanzia asubuhi hadi jioni ya kila siku” alisema a Bhatti.

Naye Meneja wa Ahmadiyya Printing Press , Dar es Salaam, Sheikh Basharat Ur Rahman Butt alisema kuwa mradi huo ulianza kwa kuchimbwa kisima cha kina kirefu ambacho ni mita 140 na uwezo wa kuzalisha maji lita 6,000 kwa saa moja .

Alisema kuwa , mradi huo wa Kihonda hadi kukamilika kwake umegharimu kiasi cha Sh milioni 150 pamoja na mwingine mdogo wa Msikiti wa jumuiya hiyo eneo la Masika.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Morogoro, Dk Kebwe aliipongeza Jumuiya hiyo kwa kuwajali watu wanyonge kuwasongezea huduma ya mradi wa maji safi na salama ambapo alitumia fursa hiyo kumwagiza Ofisa Mtendaji wa kata hiyo pamoja na Diwani kuhakikisha wanaweka utaratibu mzuri wa ulinzi wa miundombonu ya maji hayo.

Dk Kebwe alisema ,mpango wa serikali hadi kufikia mwaka 2020 huduma ya maji mijini iwe imefikia asilimia 95 ambapo kwa mkoa wa Morogoro huduma hiyo kwa mjini imefikia wastani wa asilimia 71 na kwamba mradi huo ni sehemu ya utelekezaji wa mpango wa serikali wa kufikia lengo hilo.

Nao baadhi ya wakazi wa mtaa wa Kitata , Kata ya Kihonda Maghorofani , Joyce Matemu, Winfrida Laizer pamoja na Aisha Rajabu kwa nyakati tofauti walisema kujengwa kwa kituo cha kuchota maji bure wenye bomba kumetoa unafuu wa upatikanaji maji kila siku .

Walisema mkuwa , kwa muda mrefu wamekuwa wakipata adha ya kusubiri mgao wa kila baada ya siku mbili unaotolewa na Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Manispaa ya Morogoro (MORUWASA).

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa