• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

KAMATI YA LAAC YAFANYA UKAGUZI WA MIRADI MANISPAA YA MOROGORO

Posted on: September 3rd, 2018

Kamati ya kudumu ya bunge ya hesabu za serikali za mitaa LAAC imeitaka Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kuandaa taarifa ya hesabu za miradi ya maji na barabara nakwamba muda wowote itaitwa mbele ya kamati hiyo bungeni ajili ya kuhojiwa. 

Agizo hilo lilitolewa na mwenyekiti wa kamati hiyo ya kudumu ya bunge Vedasto Ngombale Mwilu baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa kituo cha kutega na kuchujamaji pamoja na tanki la kutibu maji ya mseleleko kutoka mto Vituli yanayotumiwana wananchi wa kata ya bigwa na kingolwira manispaa ya Morogoro. 

Mwenyekiti huyo wa kamati alisema kuwa mazingira ya kwenye chanzo hicho cha maji hayaridhishi na hayako kwenye usalama kwa kuwa hakuna uzio wala ulinzi wa uhakika hivyo aliwataka MORUWASA ambao kwa sasa wanasimamia mradi huo kujenga uzito nakuimarisha ulinzi. 

Alisema kuwa kamati hiyo imekuwa ikifanya kazi baada ya kupokea taarifa kutoka kwamdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG. 

Hivyo pamoja na mambo mengine kuhusu mradi huo CAG katika taarifa yake aliyowasilisha kwa kamati hiyo alieleza changamoto za mradi huo ikiwemo ya wananchi kupasua mabomba kwa makusudi kwa lengo la kupata maji. 

“Kitendo hicho cha wananchi kupasua mabomba kwa makusudi kinazua tafsiri huwenda wananchi waliokuwa jirani na chanzo wanakosa maji na ndio maana wanaamua kupasua mambomba hayo kama njia ya kukomoa wenzao wanaonufaika na maji yachanzo hicho” alisema Ngombale Mwilu. 

Akijibu changamoto hiyo Mkurugenzi wa MORUWASA Mhandisi Nicholaus Angumbwike alisema tangu mamlaka hiyo imepokea mradi huo haijawahi kupata taarifa ya kupasuliwa kwa mabomba kwa makusudi isipokuwa inatokeaga mivujo ya kawaida hata hivyo aliahidi kuzifanyia kazi taarifa hizo. 

Naye kaimu mhandisi wa maji wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Edward Kisalu alisema kuwa mradi ulitarajiwa kuwanufaisha wananchi 8264 lakini kwa sasa kumekuwa na ongezeko kubwa la watu. 

Alisema kuwa mradi huo ulianza mwezi desemba 2014 na ulikamilika Juni 2015 na uligharimu zaidi ya Sh mil 500 fedha ambazo zilitoka serikali kuu kupitia mfuko wa pamoja wa maendeleo ya sekta ya maji. 

Mmoja wawabunge wa kamati hiyo Costantine Kinyaso alieleza wasiwasi wake kuhusu usalamana usafi wa maji kwenye chanzo hicho ambacho kiko jirani na wananchi wanaofanyashughuli mbalimbali za kibinadamu.

 

“Huku juu mlimani kwenye chanzo kuna makazi ya watu na wamejenga vyoo ambavyo viko jiranina mto, Halmashauri hebu angalieni namna ya kuwasogeza hawa wananchi waliokuwa ndani ya hifadhi ya mto vinginevyo maji haya yanaweza yasiwe salama,” alisema Kinyaso. 

Kamati hiyo pia ilikagua mradi wa barabara ya Mei mosi yenye urefu wa kilometa 5.1 ambayo ujenzi wake umegharimu Sh 11.8 bilioni na barabara yaTubuyu-nanenane- maelewano yenye urefu wa kilometa 4.6 ambayo ujenzi wake umegharimu Sh. 12.6 bilioni fedha ambazo ni mkopo kutoka benki ya dunia. 

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Morogoro Pascal Kihanga alisema kuwa ujio wa kamati hiyo katika manispaa umempa faraja kwani kwa muda mrefu kumekuwa namaneno na shutuma nyingi dhidi yake zilizokuwa zikitokewa na baadhi ya watu wakiwemo viongozi kuhusu mradi wa ujenzi wa barabara ya Tubuyu-Nanenane-Maelewano. 

“Maneno mengi yamezungumzwa lakini nashukuru kamati hii imekuja kushuhudia kwa kuona nakujiridhisha na sasa wanaweza kupima na kubaini ukweli wa maneno yaliyokuwa yakizungumzwa,” alisema Kihanga.

 Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Regina Chonjo aliahidi kutumia sheria za mazingira ili kutoa elimu kwa wananchi wanaoishi jirani na vyanzo vya maji.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa