• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

KILAKALA WAZINDUA KAMPENI YA UPANDAJI MITI 2000.

Posted on: February 19th, 2022

KATA ya Kilakala Manispaa ya Morogoro imezindua Kampeni ya upandaji wa miti 2000 ikiwa na lengo la kuhakikisha Kata hiyo inakuwa na uoto wa asili.

Kampeni hiyo imezinduliwa na Naibu Meya wa Manispaa ya Morogoro kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, Mhe. Mohamed Lukwele, leo Februari 19/2022 katika Soko la Kilakala.

Akizungumza wakati wa kampeni hiyo, Mhe. Lukwele, amesema kampeni hiyo inalengo la kuwafanya wananchi waone zoezi la upandaji miti ni sehemu ya maisha ili kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.

Kuhusu kushirikisha wanafunzi katika kampeni hiyo, Mhe. Lukwele, amesema , Kata ya Kilakala ina shule nyingi hivyo kila mwanafunzi mmoja akipanda mti wake itasaidia katika kukabiliana na changamoto hizo za kimazingira ikiwemo ukame na uhaba wa maji.

“Tumewaita wanafunzi ili muone zoezi la kupanda miti liwe sehemu ya maisha yenu shuleni, kampeni hii tunataka kila mwanafunzi ajivunie mti wake alioupanda na tutaona fahari kubwa kuwa wanafunzi weyu wanajali mazingira na tunajali nchi yetu,ukiona mvua hazinyeshi kwa wingi ujue ni mbadiliko ya tabianchi kutokana na kukosekana kwa miti ” Amesema Mhe. Lukwele.

Mwisho, Mhe. Lukwele, amewashukuru na kuwapongeza wadau mbalimbali ikiwamo SAT waliowezesha upatikanaji wa miti, Morogoro Women Voice and Connection , Ofisi ya Mazingira Manispaa ya Morogoro, Raleigh Tanzania, Wanawake na Mazingira, Moro kwanza Mazingira ,Viongozi wa vyama vya siasa, Wenyeviti wa Mitaa, Watendaji , Waalimu na wanafunzi pamoja na wananchi kwa kushiriki kikamilifu katika kampeni za upandaji miti.

Kwa upande wake, Katibu wa CCM Kata ya Kilakala, Bi. Scholastica Mwanyika , amesema amesemam zoezi kampeni hii ina umuhimu kwa sababu inalenga kuwafundisha wananchi juu ya kupanda miti.

Mwanyika , amesema kama Chama watahakikisha wanaendelea kusimamia vyema suala la mazingira kama Ilani ya CCM ya mwaka 2020-2025 inavyoeleza.

Naye Diwani wa Kata ya Kikalaka, Mhe. Marco Kanga, amempongeza Naibu Meya kwa kuzindua kampeni hiyo na kuahidi kuitekeleza.



Kanga, ameagiza shule zote za Kilakala kuhakikisha wanaitekeleza kwa vitendo pamoja na kuanzisha au kufufua klabu za mazingira ngazi ya msingi na sekondari ambayo amesema ni sehemu ya masomo.

Amesema kuwepo kwa Klabu za mazingira shuleni zitasaidia kuwafundisha vijana kupambana na athari za mabadiliko ya tabanchi na uharibifu wa mazingira kwa ujumla kwa vitendo.

"Leo tumezindua kampeni ya upandaji wa miti, tuna hatua tumezichukua kuendeleza kampeni hii ikiwamo kulinda uoto wa asili, kuendeleza utunzaji wa mazingira, kila mwanafunzi apande mti wake, shule zote kuwa na klabu za mazingira, Kila Taasisi Kilakala kupanda miti , upandaji wa miti kwa kila kaya, kwa kufanya hivyo tunaamini uoto wa asili utarejea katika Kata yetu" Amesema Kanga.

Pia, Diwani wa Viti Maalum , Mhe. Mwanaidi Ngulungu, amesema anaunga mkono kampeni hiyo kwa kuwagusa moja kwa moja wanafunzi kwani inawajega wanafunzi kupenda mazingira.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa