• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MANISPAA MOROGORO YATAKIWA KUJIKITA KUPAMBANA NA AFYA DUNI ZA WATOTO

Posted on: December 16th, 2020

HALMASHAURI ya Manispaa ya Morogoro imetakiwa kuweka nguvu katika kujikita kupambana na afya duni za Watoto.

Kauli hiyo imetolewa Desemba 16/2020 na Afisa Tawala Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Hilary Sagara, akimwakilisha Mkuu wa Wilaya katika maadhimisho ya Kilele cha Siku ya afya na Lishe iliyofanyika katika Zahanati ya Malipula Kata ya Chamwino Manispaa ya Morogoro.

“Niwapongeze sana Manispaa ya Morogoro kwa kushirikiana na wadau wa lishe, lakini nawapongeza sana watoa huduma ngazi ya jamii na ngazi ya Vituo vya kutolea huduma, kwakweli kwa haya niliyoyaona mmefanya kazi kubwa sana ya kuhakikisha Manispaa ya Morogoro inatokomeza watoto wenye udumavu, ombi langu endeleeni kupambana ikiwemo kutoa elimu mara kwa mara ili huduma hii iweze kutekelezeka vizuri katika Jamii”

Sagara, ameyataka Mabaraza yote ya Maendeleo ya Kata pamoja na Mitaa kujenga utaratibu wa kuwaalika watoa huduma ngazi za Jamii na vituo vya afya ili waweze kutoa elimu kwani huko ndipo chimbuko la afya ndipo linapojitokeza.

Aidha, amesema kuwa kauli mbiu ya mwaka huu ni lishe kwa maendeleo endelevu, hivyo jamii inapaswa kufanya kazi kwa bidii na kuweka mikakati mizuri ya uzalishaji wa chakula katika ngazi za Kaya ili Manispaa na Mkoa kwa ujumla kuweza kusonga mbele.

Mwisho, amewataka wajumbe wa kamati ya lishe katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na Wilaya kwa ujumla kusimamia na kuhakikisha wanapambana na changamoto za lishe duni kwa watoto ndani ya Halmashauri.

Kwa upande wa Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro ,Dr. Ikaji Rashidi, amesema kuwa lishe duni ni suala mtambuka na Serikali kama moja ya hatua inayorudisha nyuma kimaendeleo na mapambano dhidi ya lishe duni yamekuwa ni moja wapo ya maeneo ya kipaumbele katika mpango wa pili wa maendeleo wa miaka mitano.

“kwakuwa lishe ni suala mtambuka hatuna budi kuungana na kushirikiana kwa pamoja katika kusimamia na kuhakikisha jamii yetu inaendelea vizuri, hivyo tukishirikiana kwa pamoja tatizo hilo linaweza kuepukika ” Amesema Dr Ikaji.

Hata hivyo ,Dr Ikaji, amewashauri wazazi kuhakikisha wanawapa watoto haki zao za msingi katika lishe na kwa wakinamama wanatakiwa kuhakikisha watoto wanawapa virutubisho vizuri kwa kuwanyonyesha katika kiwango cha afya na kuacha mawazo potofu ya kuofia kupoteza uzuri wao

Afisa Lishe Manispaa ya Morogoro, Elina Kweka, amesema madhumuni ya kuadhimisha siku hiyo ni kuongeza uelewa na matokeo chanya kwa jamii ili kukabiliana na changamoto za afya na lishe zinazowakabili Watoto.

Amesema changamoto za udumavu wa Watoto katika Manispaa ya Morogoro ni asilimia 26.4%, ukondefu asilimia 3.7%, unene uliozidi kwa watoto chini ya miaka 5 ni asilimia 4.1%, upungufu wa wekundu wa damu kwa wanawake walio katika umri wa kuzaa asilimia 29.8%, upungufu wa vitamin ‘A’ kwa asilimia 33, utumiaji wa chumvi yenye madini joto asilimia 64%, unawaji wa mikono asilimia 71.5% .

Kweka, amesema miongoni mwa shughuli mbali mbali za lishe zinazotolewa katika vituo vya kutolea huduma za afya zinazolenga makundi mbali mbali Wanawake, wanaume , vijana rika balehe , wadau mbalimbai , viongozi wa dini na asasi za kiraia ni pamoja na utoaji wa matone wa vitamin A, dawa za minyoo na utambuzi wa hali ya lishe kwa watoto chini ya umri wa miaka 5,

“Huduma hizi tumeanza kuzitoa kuanzia tarehe 01-31 mwezi Desemba 2020 katika vituo vyetu 47 vinavyotoa huduma za uzazi na Mtoto, huma hii hutolewa mara 2 kwa mwaka yaani mwezi wa 6 na mwezi wa 12, lakini elimu hii ya huduma tumezitoa kwa njia ya vyombo vya habari ikiwamo redio, TV , vikundi malezi vilivyopo ngazi za Mitaa, kuwaunganisha watoa huduma ngazi ya jamii katika vituo vya afya vilivyopo katika Ofisi ya Kata , utoaji wa huduma magonjwa yasiyoambukizwa yanayohusiana na lishe, elimu katika makao ya Watoto na kutoa mafunzo kwa watoa hudma na vikundi vya wakulima kwa kushirikiana na wadau’’ Amesema Kweka.

Naye , Mratibu wa mradi wa Lishe Endelevu Mkoa wa Morogoro, Mariam Mwita, amesema suala la lishe ni mtambuka hivyo jamii kwa kushirikiana na wadau mbali mbali pamoja na Serikali kuhakikisha wanajenga Vizazi vyenye watoto wenye afya na lishe bora ili kuepuka udumavu.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa