• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MANISPAA YA MOROGORO KUJENGA KITUO CHA BURUDANI KWA WANAMICHEZO

Posted on: October 3rd, 2020

MANISPAA ya Morogoro ipo kwenye mpango wa kujenga Kituo cha Burudani ambacho kitakuwa na lengo la kuwakutanisha Wanamichezo na wasanii kwa pamoja .

Kauli hiyo ya ujenzi wa Kituo cha Burudani , imetolewa leo na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro , Mhe. Bakari Msulwa, leo Oktoba 03, 2020 wakati wa kujumuika katika mazoezi ya pamoja na wadau wa michezo kwenye Viwanja vya Gymkhana Manispaa ya Morogoro.

Akizungumza na Waandishi wa habari, Msulwa, amesema Ujenzi huo ni mpango ambao upo kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

“”Nimeongea na Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, amesema wao wana mpango huo, lakini ujenzi huo wa kituo cha burudani hautaishia katika michezo tu bali kituo hicho kitakuwa cha uwekezaji, tunataka wanamichezo wawe na kijiwe chao lakini sio kwa Manispaa ya Morogoro pekee bali hata Morogoro Vijijini lazima wawe na mpango huo huo wa kujenga Kituo cha Burudani, “”Amesema DC Msulwa.

Mbali na hayo,amewataka Wanamichezo kuadhimisha siku ya Mwalimu Nyerere kwa kujumika pamoja katika eneo la mradi wa Nyama Choma Manispaa ya Morogoro kwa ajili ya kusheherekea siku hiyo muhimu kwa pamoja ikiwamo kula na kunywa kwa ajili ya kujenga afya zaidi.

“”Tumekubaliana na Mkurugenzi hapa kwamba siku hiyo ndiyo inategemea mradi wa ujenzi wa nyama choma kuzinduliwa hivyo sisi wanamichezo kwa pamoja tutakutana hapo, tutakunywa supu na nyama choma, pamoja na vinywaji, baada ya hapo tunaongea na wadau wa michezo wakati tukiwa tumeshiba waone namna ya kuweza kutusaidia, kwahiyo tunataka siku hii iwe sherehe kubwa kwetu “”Ameongeza DC Msulwa.

Msulwa, amesema yote yanayofanyika ni kutengeneza mpango kazi utakaoweza kuwaunganisha wadau wote wa Michezo Wilaya ya Morogoro katika kuendeleza na kukuza vipaji vyao nap engine kuzalisha ajira kwa ajili ya maisha yao.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, amesema siku ya Mwalimu nyerere atatoa ngómbe mmoja kwa wanamichezo .

“Niwaombe Wanamichezo tujitokeze kwa wingi, ngómbe mmoja siwezi kumla peke yangu, nawakaribisha sana katika mradi wetu mpya wa nyama choma nanenane , michezo ni afya na michezo ni ajira, Morogoro ya Viwango inawezekana tukishikana kwa pamoja”Amesema Lukuba.

Naye, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Bi. Rehema Bwasi, amesema huu ni mwanzo , hivyo amewataka Wanamichezo kutokata tama kwani yapo mambo mazuri yanakuja.

“Nimefurahi kukutana nanyi tena katika juma hili, hii ni mara ya pili, tumpongeze sana Mkuu wetu wa Wilaya kwa kutuletea jambo hili katika kudumisha michezo katika Wilaya yetu ya Morogoro, niwaombe wanamichezo hiki ambacho Mkuu wetu wa Wilaya amekianzisha tuendelee kukidumisha, tunataka Morogoro ya Viwango iwe ya kweli na kurudisha heshima yetu katika Michezo “”Amesema Bwasi.

Katika hatua nyingine, Bwasi, amesema kuwa , muamko ni mzuri kwani kitendo cha Msanii mkubwa kama Rayvanny kuunga mkono suala la michezo na burudani inaonesha ni jinsi gani kampeni hiyo inakwenda kufanikiwa.

Katika hatua nyengine, Mbunge Mteule wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki , Mhe. Hamisi TaleTale maarufu kwa jina la Babu Tale , amewataka Wanamichezo kuendelea kutengeneza vipaji kwani Morogoro ni Mkoa ambao umejaliwa kuwa na vipaji vingi vya michezo.

“Niwaahidi tu wana Morogoro, tutashikana bega kwa bega kuhakikisha tunainua suala la michezo na sio katika michezo pekee bali hata kwenye Sekta ya elimu kama alivyozungumza Mkuu wa Wilaya”” Amesema Mhe. Tale.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa