• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MANISPAA YA MOROGORO KUWAFIKISHA MAHAKAMANI WAFANYABIASHARA WALIOGOMA KULIPA KODI YA HUDUMA.

Posted on: February 5th, 2018

BARAZA la madiwani la halmashauri ya Manispaa ya Morogoro limeadhimia azimio la kuwafikisha mahakamani wafanyabiashara wakubwa na wa kati waliogomea kwa muda mrefu kulipa jumla ya kiasi cha fedha inayokadiriwa kufikia Sh bilioni 2.1 zinazotokana na kodi ya ushuru wa huduma ( Service Levy ) iliyopo kisheria.

Wafanyabiashara hao wamegoma kulipa kodi ya ushuru wa asilimia 0.3 iliyopitishwa na Bazara Madiwani kwenye vikao vyake vilivyopita, huku wakishinikiza kuwa tayari kulipa kwa kiwango cha asilimia 0.1, kinyume na maamuzi yaliyopitishwa na Baraza la Madiwani.

Azimio la kuwafikisha mahakamani wafanyabiashara hao lilipitishwa katika kikao cha kawaida cha baraza la Madiwani kilichofanyika hivi karibuni baada ya Mkurugenzi wa Manispaa  John Mgagula, kuwasilisha taarifa ya mwenendo usio wa kulidhisha wa ukusanyaji wa mapato.

Katika taarifa yake kwa Baraza hilo alisema wafanyabishara wakubwa wanadaiwa kiasi cha Sh bilioni 1.7 na wamegoma kutolipa kodi kwa kiwango cha asilimia 0.3 huku wenyewe wakitaka walipe kiwango cha asilimia 0.1 ambao Ofisi yake imekataa hoja hiyo.

“ Sasa hivi kuna mgomo wa wafanyabiashara wakubwa na wakati , hawataki kulipa kiwango cha ushuru wa huduma cha asilimia 0.3 kilichopitishwa na baraza hili, wamegoma na wamesema wako tayari kulipa asilimia 0.1” alisema Mgalula na kuongeza.

“ Mimi  kama Mkurugenzi wa Manispaa kiwango hicho hakiwezi kupunguza ,nina leta kwako Mstahiki Meya ili baraza lako lilidhie twende mahakamani kuwashitaki ” alisema Mgalula.

Nao baadhi ya Madiwani wa baraza hilo, Mabula Lusewa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA ) alisema kuwa Katibu wa Baraza ambaye ni Mkurugezi amelileta kwetu kutuomba kuruhusu kwenda mahakakani na jambo hilo ni budi lipewe baraka kama tunahuitaji mapato kwa maendeleo yetu sote.

Hata hivyo baadhi ya madiwani Juma Tembo , Mudhihir Shoo na Amir Nondo kwa nyakati tofauti walisema suala hilo linahitaji busara zaidi , kabla ya kuchukua uamuzi wa kwenda mahakamani.

Pamoja na hoja hizo, Mkuu wa wilaya ya Morogoro, Regina Chonjo ambaye alialikwa katika Baraza hilo alisema , Serikali ya Wilaya inaona uamuzi uliochukuliwa na baraza la madiwani kwenda mahakamani uko sahihi, kwani jambo hilo lipo kisheria kutokana na halmashauri kutoza asilimia 0.3 na si zaidi ya hapo .

“ Nikiwa natakiwa nisimamie maendeleo ya Manispaa hii, haiingii akilini jambo lipo kisheria bado linajadiliwa , sheria inawataka walipe kuanzia asilimia 0.1 hadi kufikia 0.3 na si zaidi ya hapo na Baraza hili lilipitisha azimio wafanyabiashara walipe asilimia 0.3 baada ya kufanyika utafiti na wataalamu “ alisema Chonjo.

Hivyo aliunga mkono azimio la kuwafikisha mahakamani wafanyabiashara hao na kushauri kuwa endapo mfanyabiashara mmoja mmoja anayo malalamiko yake ni vyema ayawasilishe kwenye mamlaka za Manispaa ili yafanyiwe kazi na si kuchukua uamuzi wa kugoma kwa kuwa wengi wao wanalipa bila matatizo kodi ya Mamkala ya Mapato Tanzania (TRA).

Kufuatia hoja hizo , Meya wa Manispaa , Pascal Kihanga aliwahoji madiwani hao juu ya azimio la kuwafikisha mahakamani , na wote kwa kauli moja walipitisha azimio hilo la kuwafungulia kesi wafanyabiashara wote wakubwa na wa kati waliogoma kulipa kodi ya huduma wa asilimia 0.3 ulioweka kisheria.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa