• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MANISPAA YA MOROGORO YAFUNGUA MAFUNZO YA KINGA TIBA YA DAWA YA KICHOCHO KWA WALIMU WAKUU SHULE ZA MSINGI NA WALIMU WA AFYA

Posted on: November 10th, 2022

HALMASHAURI ya Manispaa ya Morogoro imefungua mafunzo kwa walimu wakuu wa shule za Msingi ikiwamo na shule binafsi , walimu wa afya kwa ajili ya kuwaandaa katika kusimamia zoezi la ugawaji wa dawa za kichocho kwa wanafunzi wenye umri wa miaka 5-14 linalotarajia kufanyika tarehe 15/11/2022.

Akizungumza katika ufunguzi huo, Kaimu Mganga Mkuu wa Manispaa ya Morogoro, Bertha Mahanga, amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha zoezi hili la ugawaji wa dawa linatekelezwa vizuri ili kila mtoto/mwanafunzi aweze kupewa dawa hizo.

Mahanga, amesema Manispaa imejipanga vizuri na imeweka malengo mkakati ya utekelezaji wa mpango wa kugawa dawa Shuleni ikiwamo upatikanaji wa huduma hiyo katika vituo vya huduma ya afya pamoja na kujenga uwezo wa utekelezaji wa mpango huo kwa jamii ili jamii iwe na afya bora.

" kichocho husababishwa na minyoo inyoitwa jamii ya Schistosoma ambao unaenezwa na konokono kwa kutoa vimelea kupitia maji yaliyotuama, lakini athari yake husababisha damu kutoka kwenye njia ya mkojo na choo, na baadae inaweza kusababisha saratani ya tumbo, kibofu cha mkojo na ini" Amesema Mahanga.

Naye Mratibu wa Magonjwa yasiyopewa kipaumbele Manispaa ya Morogoro, Dr.Warialanga Nnko,amesema kuwa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ni magonjwa ambayo yamo ndani ya jamii zetu, hivyo kwa mpango huu wa ugawaji wa dawa hizi utaleta matokeo chanya na kuwakinga watoto na kichocho.

" Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ni magonjwa ambayo yamo ndani ya jamii ni usubi, Matende na mabusha, Trakoma, kichocho na minyoo ya tumbo, hivyo katika kuona kasi ya maambukizi ya ugonjwa wa kichocho inapungua , Serikali ikaona kuja na mpango wa dawa kwa watoto miaka 4-15 kwani wao wapo katika uhatari wa kupata ugonjwa huo kwa haraka kutokana na kuogelea katika madimbwi ya maji " Amesema Nnko.

Mmoja wa watoa mafunzo , Dr. Caroline Sakaya, amezitaja njia za kujikinga na magonjwa ikiwamo kutumia dawa za kutibu na kudhibiti magonjwa haya ambazo hutolewa kila mwaka kwa jamii iliyoathirika, kuzingatia usafi wa uso na mwili, usafi wa mazingira, kutokuoga kwenye maji yasiyo safi na yaliyotuama (bwawa), kujikinga kuumwa na inzi au mbu, na kutoa elimu ya afya ya jamii.

Katika mafunzo hayo waalimu walipewa majukumu ikiwamo kutoa elimu ya afya kuhusu manufaa na maelekezo ya umezaji dawa husika kwa kiongozi wa shule, wazazi, na wanafunzi, kuandikishwa walengwa (wanafunzi) kwenye rejista, kuaandaa chakula kwa ajili ya wanafunzi kabla ya kumeza dawa na Dawa hiyo imezwe ndani ya masaa mawili baada ya kula chakula.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa