• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MANISPAA YA TEMEKE YAIPONGEZA MANISPAA YA MOROGORO KWA USIMAMIZI MZURI WA SOKO LA KIMKAKATI LA CHIFU KINGALU

Posted on: October 15th, 2021

HALMSHAURI ya Manispaa ya Temeke imeipongeza Manispaa ya Morogoro kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo ikiwamo mradi wa Soko Kuu la Kisasa. pamoja na Stendi ya mabasi Msamvu.

Akizungumza na Waandishi wa Habari , Oktoba 15/2021 , Mstahiki Meya wa Manispaa ya Temeke , ambaye ndiye kiongozi wa msafara, Mhe. Abdallah Mtinika amesema kasi ya miradi ya maendeleo ya Manispaa ya Morogoro imewafurahisha hivyo amelitaka Baraza la Madiwani Manispaa ya Temeke kuhakikisha wanapo rudi nyumbani waanze kufanyia kazi kwa kile walichojifunza.

Amesema kuwa, Manispaa ya Morogoro inahitaji kupongezwa sana kwani wamepiga hatua kubwa huku wakionesha thamani ya fedha katika miradi na wamekuwa mfano wa kuigwa hususani katika miradi hiyo na kuifanya manispaa  kuongeza miradi mingine katika pato lao la ndani.

Mhe. Mtinika , amefurahishwa zaidi jinsi Manispaa hiyo ilivyoweka vipaumbele hususani katika kuwahamisha wafanyabiashara kwa maridhiano na kuwapa kipaumbele mara baada ya kukamilika kwa mradi huo.

Aidha, amefurahishwa zaidi kuona Watu wenye uhitaji maalumu wametengewa maeneo yao maalumu, jambo ambalo linalenga kuleta usawa kwa wote na kuendeleza adhima ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, ya kuwaendeleza walemavu , wakina Mama pamoja na vijana.

"'Niwapongeze viongozi wa Manispaa ya Morogoro kwa kushirikiana na Baraza la Madiwani na Wataalamu, kazi inaonekana , kwakweli katika miradi yenu kuna vitu vingi tumejifunza, sisi kwetu tuna miradi mingi lakini tumejifunza jinsi ya kuendesha mradi wa Soko na tukirudi tutakwenda kukaa na wafanyabiashara kuona jinsi gani tutawasogeza kwa maridhiano kujenga soko nje ya mji haitakuwa biashara nzuri kwetu bora tujenge katikati ya mji ili tuweze kupata mapato, kingine katika mradi wa stendi ya Msamvu tumeona wakaguzi wa kimataifa wanavyofanya kazi yao kwakweli inaonesha ni jinsi gani Manispaa yenu mlivyo karibu na Serikali pamoja na Chama Tawala CCM" Amesema Mhe. Mtinika.

"Ukiangalia Manispaa yetu ya Temeke , tunataka kuibua miradi mikubwa lakini tunahitaji kukusanya kodi katika miradi hiyo, hivyo lengo letu kubwa kuja hapa ni kuona namna gani tutapata uzoefu na kujua wenzetu wanatumia aina gani ya ukusanyaji wa mapato na usimamizi wa miradi ili nasisi tuweze kufanya kama wanavyofanya wao japo sisi mapato yetu makubwa lakini kujifunza hakuna mwisho hata mtoto anaweza kujifunza kwa mkubwa " Ameongeza Mhe. Mtinika .



Hata hivyo, amesema watamshauri Mkurugenzi pamoja na Baraza la Madiwani la Halmshauri ya Manispaa ya Morogoro , kuhakikisha mara baada ya kukamilika kwa miradi ya maendeleo waweke uongozi mzuri ambao wataamua katika Baraza lao na utakaokuwa unauwezo wa kukusanya fedha ili Manispaa iweze kuendesha miradi mingine.

Amesema siku zote katika kuhitaji maendeleo lazima ujifunze kwa mwenzako maana rasilimali pesa inakuwa ndogo kuliko idadi ya watu, hivyo wamejifunza jinsi ya kuendesha miradi vizuri, isije tena ikwawa wameibua miradi,harafu miradi hiyo ukaleta migogoro na kutokuwa na tija kitu ambacho hakitawasaidia katika kufikia malengo yao ya kukusanya kodi.

Kwa upande wa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro, Mhe. Pascal Kihanga, , ameipongeza Manispaa ya Temeke kwa kujitolea kuja kujifunza namna ya kuendesha miradi na jinsi ukusanyaji wa mapato.

Mhe. Kihanga, amesema kujifunza sio dhambi hivyo wataendeleza ushirikiano huo pindi pale watakavyohitajika kufanya hivyo kwa Ustawi wa Maendeleo ya Tanzania na Wananchi kwa Ujumla.

Amesema kuwa kujifunza ni njia ya kupata maendeleo zaidi ,hivyo kwa kupitia mafunzo hayo Manispaa ya Temeke watanufaika sana na wataimarisha mifumo ya kodi na kuiletea Manispaa yao Mendeleo.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Michael Waluse, amesema kuwa , Manispaa ya Morogoro ipo chini kimapato ukilinganisha na Manispaa nyengine za Mjini kama kwenye Majiji makubwa , lakini wanajitahidi sana kufuatilia vyanzo vya mapato , amewahahakishia ushirikiano na kunufaika na lengo la ziara yao yenye kulenga kuwajengea uzoefu na kujua mbinu wanazotumia za ukusanyaji wa mapato.

" Kweli tumewapokea ndugu zetu wa Manispaa ya Temeke kutoka Jiji la Dar Es Salaam, kwa ajili ya kuja kujifunza hapa kwetu, matumaini yangu ni kwamba tangia walivyokuja ni tofauti na sasa baada ya kuondoka, lakini tunachowaambia mafanikio yetu ni kuwa na nidhamu katika matumizi ya fedha za miradi , hivyo tunakusanya fedha nyingi lakini hizi fedha tunazipeleka kwenye miradi ya wananchi na miradi hiyo inaonekana, lakini Manispaa ya Morogoro tumekuwa na miradi mikubwa matarajio yetu baada ya miradi hii kukamilika tutakusanya pesa na tutazielekeza katika kuibua miradi mengine ya maendeleo"Amesema Waluse.


Waluse, amesema ili kufikia lengo katika ukusanyaji wa kodi ni lazima uheshimu misingi ya matumizi mazuri ya pesa pamoja na kuwekeza katika miradi ya wananchi.

Naye Mbunge wa Jimbo la Temeke, Mhe. Dorothy Kilave, ameipongeza Manispaa ya Morogoro kwa hatua nzuri za usimamizi wa Soko lakini katika mfumo mzima wa kuwapanga Machinga na kuwaweka sehemu moja.

"Wenzetu wamefanya jambo kubwa sana, tuna cha kujifunza hapa, na sisi tukirudi tutachukua njia zote nzuri ambazo wenzetu wa Manispaa ya Morogoro wamezitumia kwanza kusimamia Soko kubwa kama hili na jinsi walivyoweza kuwapanga Machinga katika mpangilio mzuri, niupongeze Uongozi wa Mkoa, Wilaya ya Morogoro na Manispaa kwa hatua kubwa za kuwawekea Machinga Mazingira rafiki ya kuifanyia biashara zao za kujiingizia kipato " Amesema Mhe. Kilave.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa