• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MANISPAA YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KWA HALMASHAURI YA WILAYA MOROGORO

Posted on: April 29th, 2024

Asubuhi tarehe 28.04.2024, Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Morogoro ndugu Emmanuel Mkongo, amemkabidhi Mwenge wa Uhuru pamoja na wakimbizaii wa kimkoa na wa kitaifa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Morogoro ndugu JoanFaith Katalaiya.

Awali alipokuwa akizungumza na umma uliokuweo wakati wa makabidhiano hayo, ndugu Mkongo amesema jana asubuhi Mwenge wa Uhuru ulipowasili kwenye Manispaa ya Morogoro, ulikimbizwa umbali wa kilomita 94, kwenye miradi 10 ya maendeleo , yenye thamani ya shilingi bilioni 3.6, ambazo ni fedha kutoka Serikali Kuu, Mapato ya Ndani ya Manispaa na michango ya wananchi wa Manispaa ya Morogoro.

“Katika miradi kumi iliyopitiwa na Mwenge wa Uhuru, mitano ilionwa, miwili iliwekewa jiwe la msingj kila mmoja, na miwili ilizinduliwa” alifafanua Mkongo.

Kwa upande wake Mkufunzi wa Mwenge wa Uhuru Kitaifa Kapten Musa Mohamed Ngomambo amempongeza mbunge wa jimbo la Morogoro Mjini Mheshimiwa Dkt. Abdul-Aziz Abood pamoja na mbunge wa viti maalumu wa jimbo hilo Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma kwa kushiriki kikamilifu katika Mapokezi na safari nzima ya kuukimbiza Mwenge wa Uhuru mpaka kuukabidhi kwenye jimbo la Morogoro Vijijini.

Kapten Ngomambo amesema kuwepo kwa wabunge hao kwenye mbio za Mwenge wa Uhuru ndani ya Manispaa ni faraja kubwa kwake na wenzake, kwa sababu waheshimiwa wabunge ndio ambao huisemea bungeni miradi ya maendeleo ambayo hutekelezwa na Halmashauri kwenye majimbo yao.

Naye Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa (2024) ndugu Godfrey Mnzava ameipongeza Manispaa ya Morogoro kwa kuwa na Mapokezi mazuri ya Mwenge wa Uhuru, an miradi mizuri ya maendeleo ambayo Mwenge wa Uhuru imeitembelea.

Ndugu Mnzava ameitaka Manispaa ya Morogoro kuendelea kusimamia miradi ya maendeleo na kuhakikisha inaleta tija kwa wananchi wa Manispaa hiyo.

Miongoni mwa miradi ya maendeleo iliyopitiwa na Mwenge wa Uhuru kwenye Manispaa ya Morogoro ni pamoja na mradi wa Zahanati ya Kauzeni kata Kauzeni, mradi wa upandaji wa miti kata Mindu, mradi wa jengo la wafanya biashara wadogo (machinga) kata ya Uwanja wa Taifa, miradi miwili ya maji, mradi wa kikundi cha vijana wanufaika wa mkopo wa asiimia kumi, na mradi wa ujenzi wa barabara ya zege ya Kichangani.

MWISHO

 




[U1]




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa