• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MBUNGE MZERU ATIMIZA AHADI, AKABIDHI MIFUKO 100 SHULE YA SEKONDARI LUPANGA, MANISPAA YATOA NENO.

Posted on: January 18th, 2022

MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Morogoro kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM, Mhe. Norah Mzeru, ametimiza ahadi yake ya kukabidhi Mifuko 100 ya Saruji Shule ya Sekondari Lupanga iliyopo Kata ya Kilakala Manispaa ya Morogoro kwa ajili ya ukarabati wa madarasa ambayo yameonekana kuchakaa.

Akizungumza kwa niaba ya Mbunge Mzeru, Katibu wa Mbunge huyo , Ismail Kifaru, amesema kuwa mifuko aliyotoa Mhe. Mzeru ametumia fedha zake binafsi kununua mifuko hiyo lengo likiwa ni kusaidia kufanikisha ukarabati wa madarasa ambayo yameonekana kuchakaa ili yaendane na madarasa mapya na wanafunzi wasome katika mazingira rafiki yenye kuvutia.

Kifaru, amewataka wanafunzi wa shule ya Lupanga kusoma kwa bidiii ili waweze kufanya vizuri katika mitihani yao na atakuwa mstari wa mbele kuwasaidia katika kutatua changamoto zinazo wakabili kwa kadri watakavyoweza kujaliwa.

Katika hatua nyingine, Kifaru, amewapongeza wanafunzi waliofanya vizuri pamoja na kushukuru waalimu kwa kujitoa kwao katika kufundisha na kuongeza ufaulu shuleni hapo.

Naye Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro ambaye pia ni Afisa Taaluma Sekondari Manispaa ya Morogoro, Muhaiki Deogradia, amempongeza Mhe. Mzeru kwa mifuko hiyo ya saruji na kumuahidi mifuko hiyo itaenda kufanya kazi tarajiwa.

Naye Diwani wa Kata ya Kilakala, Mhe. Marco Kanga, amemshukuru Mhe. Mzeru na huku akisema kuwa kitendo cha Mhe. mzeru kutoa mifuko hiyo ya saruji kinaonesha ni jinsi gani Mhe. Mzeru anaunga mkono Jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassani ya kujenga miundo mbinu bora ya elimu na kuwezesha wanafunzi kusoma bila shida.

Hata hivyo, Mkuu wa Shule ya Lupanga, Flora Ndunguru, amesema kuwa Msaada huo utasaidia kutatua changamoto waliyo nayo ya uchakavu wa madarasa .

Amesema wanatarajia kupokea wanafunzi 274 , hivyo kwa madarasa ambayo watayakarabati basi yatasaidia wanafunzi kusoma katika mazingira rafiki na kuongeza ufaulu kwa wanafunzi wanaotarajia kufanya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2022.

Kwa upande wa mwanafunzi wa kidato cha kwanza aliye jitambulisha kwa jina la Theresia Minja, ametoa pongezi kwa Rais Samia na kumshukuru Mbunge Mzeru , kwa moyo alioonyesha kujitoa kuwasaidia kutatua changamoto hiyo na kumuahidi kuwa watasoma kwa bidii na Kufaulu kwa asilimia 100 katika mitihani yao pamoja na kuongeza ufaulu shuleni hapo.

Ikumbukwe ahadi ya Mhe. Mzeru, ya kutoa mifuko hiyo 100 ya Saruji, ilitokana na ziara yake ya kikazi aliyoifanya Januari 17/2022 katika kutembelea madarasa mapya yaliyojengwa na fedha za Maendeleo na ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO-19 .

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa