• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MEYA KIHANGA AWATAKA VIONGOZI WA VYAMA VYA USHIRIKA KUFANYA KAZI KWA KUZINGATIA UADILIFU

Posted on: June 22nd, 2022

MSTAHIKI Meya wa Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga, amewataka Viongozi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Morogoro kufanya kazi kwa kuzingatia uadilifu.

Kauli hiyo ameitoa leo Juni 21/2022 katika Jukwaa la Maendeleo ya Ushirika Mkoa wa Morogoro lililofanyika katika Ukumbi wa Savoy Morogoro Manispaa.

Akizungumza katika Jukwa hilo, Mhe. Kihanga, amesema kutofanya kazi kwa kuzingatia uadilifu kuna pelekea ubadhilifu wa fedha pamoja na migogoro ndani ya ushirika.

“Lazima mfanye kazi kwa uadilifu , msiruhusu migogoro,mkiwa na migogoro hata wale wanaotaka kutoa misaada hawatawaletea tena, simamieni miiko ya Uongozi ili Wanachama wenu waweze kunufaika na Ushirika huu” Amesema Kihanga.

Aidha, Kihanga, amewataka Viongozi kufanya kazi kwa kusimamia sheria na kanuni badala ya kufanya kazi kwa mazoea jambo ambalo halitawafikisha mbali na kutofika mafanikio au malengo waliojiwekea.

Hata hivyo, amewataka Viongozi wa Vyama vya Ushirika kuhakikisha katika Mikutano yao agenda kubwa iwe uadilifu ili kujenga uwaminifu kwa wanachama wao.

Kuhusu changamoto ya vyama vya mazao, amezitaka Taasisi za kifedha kuvitembelea vyama hivyo na kuweza kutatua changamoto zao.

Naye Mwenyekiti wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Morogoro, Idd Rajabu, amesema lengo la Mkutano huo wa Jukwaa la Vyama vya Ushirika ni kuwakutanisha wana Ushirika na wadau wake kwa ajili ya kujengeana uwezo na uzoefu ili kujenga Ushirika Imara na wenye nguvu.

Kwa upande wa Mrajisi wa Vyama Vya Ushirika Mkoa wa Morogoro, Keneth Shemdoe, amesema kazi kubwa ya kufanya katika kuimarisha Vyama Vya Ushirika ni kutoa elimu na ushauri, usimamizi na ukaguzi .

Shemdoe ,amesema kuwa katika Mkoa wa Morogoro kuna jumla ya upungufu wa Maafisa Ushirika 22, hivyo kuna kila haja ya kuweza kupata wataalamu hao ili kuimarisha vyama hivyo kwa ngazi za Halmashauri.

Mwisho, Shemdoe, amesema kwa sasa jukumu kubwa la Jukwaa la Vyama Vya Ushirika ni kuimarisha Masoko na uwezeshaji wa wananchi kiuchumi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa