• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MHE.AMIR NONDO AZINDUA KAMPENI YA UPANDAJI MITI MANISPAA YA MOROGORO

Posted on: April 12th, 2018

Mwenyekiti wa Kamati ya Mipangomiji na Mazingira Manispaa ya Morogoro Mhe.Amiri J.Nondo leo tarehe 12/04/2018 amezindua rasmi kampeni ya upandaji miti.Uzinduzi huo umefanyika katika shule ya Msingi Mkundi.

Mhe. Nondo akizungumza wakati wa zoezi hilo amesema  kwa kuzingatia waraka wa Serikali,Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa wiki hii ya upandaji miti ambayo uzinduzi wake umefanyika leo jumla ya miche 5000 ya miti mbalimbali ikiwemo mitiki,mikongo na migrivelia itapandwa katika kata ya Mlimani(miti 1,000) na kata ya Mkundi (miti 4000).

Mhe. Nondo amesema kwa kuzingatia kauli mbiu ya mwaka huu inayosema "Tanzania ya kijani inawezekana,Panda miti kwa Maendeleo ya Viwanda" hivyo upandaji miti utapendeza sana kwa maendeleo ya viwanda iwapo mazingira yatatunzwa na kuweza kuwavutia wawekezaji mbalimbali wa viwanda vikubwa , vya kati na vidogo ,lakini pia kwenye biashara za mahoteli,nyumba za kulala wageni,maduka,masoko na hivyo kuchangia mapato katika Manispaa ya Morogoro.

Aidha ameeleza kampeni ya upandaji miti iliyozinduliwa iwe endelevu na iwashirikishe wananchi wote wa Manispaa ya Morogoro katika maeneo wanayoishi,pamoja na sekta zote binafsi ili kutoa fursa walizonazo katika kupanda miti kwa wingi.

"Uzinduzi wa upandaji miti uende sambamba na udhibiti wa ongezeko la watu lisilowiana na mahitaji ili kudhibiti ongezeko la shughuli za kibinadamu zinazochangia uchomaji moto hovyo,ukataji wa misitu kwaajili ya kilimo kisichokuwa endelevu,ujenzi wa makazi,nishati kama mkaa,kuni na mbao na uwindaji wa wanyama"ameeleza Mhe. Nondo.

Aidha ameshauri jitihada zaidi ziongezeke ili kunusuru hali ya uharibifu a maliasili na mazingira unaoendelea nchini ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi.Pia amesisitiza suala la uhifadhi wa uoto wa asili na mapori ya akiba yaliyopo kwenye Manispaa yetu lipewe umuhimu unaostahili kwa mfano maeneo ya hifadhi yaliyopo kwenye milima ya Uluguru,eneo la Nguru ya Ndege,na eneo la msitu wa Mindu.

Naye Diwani wa Kata ya Mkundi Mhe Hilda Benedict ametoa shukrani kwa kuteua kata hiyo kufanyia uzinduzi na kusisitiza wananchi kuitunza na kuithamini miti hiyo itakayopandwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa