• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MKURUGENZI MANISPAA MOROGORO AWAPONGEZA WAZAZI KWA KUCHANGIA MAENDELEO YA SHULE.

Posted on: January 6th, 2020

MKURUGENZI wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, amewapongeza Wazazi wanaowasomesha watoto wao shule ya Msingi Mkundi kwa kujitoa na kusaidia ujenzi katika shule hiyo.

Akizungumza leo Januari 6, 2020 mara baada ya kutembelea shule hiyo kwa ajili ya kuangalia mwitiko wa wanafunzi walioandikishwa kuanza darasa la kwanza mwaka 2020, kufuatia mpango wa elimu bure bila malipo.

Amesema kuwa, kitendo cha Wazazi hao kuchangia kila mmoja Shilingi elfu 15 na tofali 3  ni makubaliano  yaliyofanyika katika vikao na yakaandikiwa mihtasari kwaajili ya kupata kibali cha michango  na hii ni baada ya Wazazi hao kuona wingi wa wanafunzi na changamoto ya madarasa, hivyo amekitaka kitendo hicho kiwe mfano wa kuigwa kwa wazazi wengine ikiwa ni mapokeo mazuri ya wazazi kutambua umuhimu wa kusaidiana na Serikali kwa Maendeleo ya Watoto wao.

"Hii ni hatua nzuri sana, na imeondoa ile dhana ya Wazazi kuachia Serikali peke yake baada ya kuona elimu inatolewa bure, ndugu zangu kuchangia sio dhambi, Mhe. Rais Dkt. John Magufuli, amekuja na mpango wa elimu bure lakini sio kwamba kila kitu uiachie Serikali kwani elimu ina pembe tatu Mwanafunzi, Mwalimu pamoja na Mzazi, tukiwa kitu kimoja naamini hata matokeo ya ufaulu wa watoto wetu utaongezeka na kutengeneza Taifa lenye kuleta matokeo chanya hususani katika kuelekea uchumi wa kati na Tanzania ya Viwanda" Amesema Sheilla.

Aidha ameipongeza Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Mhe. Rais Dkt John Magufuli kwa kubuni na kutekeleza mpango wa elimu bure bila malipo, jambo ambalo limesaidia sana wazazi kuwaandikisha watoto wengi tofauti na kipindi cha nyuma na asilimia kubwa ya wanafunzi imeongezeka katika uandikishwaji.



Kwa upande wao, Wazazi nao walichukua nafasi ya Kumpongeza Mhe. Rais Dkt. John Magufuli huku wakisema elimu bure imewasaidia na sasa hivi watoto wengi wameandikishwa na wanasoma lakini wameomba kuangaliwa kwa jicho la tatu na kusaidiwa pale watakapo ishia katika jitihada zao za kutatua changamoto shuleni.

Naye Afisa Elimu Msingi Manispaa ya Morogoro, Abdul Buhetty, amempongeza Mkurugenzi kwa kutembelea shule hiyo lakini amemuomba kutatua changamoto zilizopo katika shule za msingi ili kuongeza viwango vya ufaulu na kuing'arisha Manispaa katika mitihani Kitaifa.

Amesema Shule ya Msingi Mkundi, kabla ya uandikishwaji wa wanafunzi wapya ilikuwa na jumla ya wanafunzi 2042 na sasa bado zoezi la uandikishwaji unaendelea.


Mbali na kutembelea Shule ya Msingi Mkundi pia ametembelea Shule ya Sekondari Kihonda Maghorofani.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa