• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MKURUGENZI MANISPAA YA MOROGORO AGAWA NDOO ZA MAJI KATIKA MAKAZI YA KULELEA WATOTO PAMOJA NA WAZEE WASIOJIWEZA KWA AJILI YA KUJIKINGA NA UGONJWA WA CORONA

Posted on: April 1st, 2020

MKURUGENZI wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, amevigawia jumla ya Vituo 7 vya kulelea watoto yatima na wanaoishi katika Mazingira magumu pamoja na Wazee wasiojiweza ndoo za kunawia , sabuni pamoja na mabeseni ya kukingia maji machafu kwa ajili ya kujikinga na Ugonjwa wa CORONA.

Akizungumza na kukabidhi ndoo hizo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Afisa Ustawi wa Jamii Manispaa ya Morogoro, Sidina Mathias, amesema ndoo hizo alizo zitoa Mkurugenzi ni moja ya jitihada za kuunga Mkono Serikali kwa ajili ya mapambano dhidi ya Ugonjwa wa CORONA .


Amesema kuwa, kwa kutambua umuhimu wa Makazi hayo ya Watoto wanaoishi katika mazingira magumu pamoja na Wazee wasio jiweza , Mkurugenzi ameona ni bora kuwapelekea ndoo ili zile pesa wanazopata ziweze kuwasaidia katika matumizi ya huduma nyengine.


“Leo tunatoa ndoo hizi kwa Makazi ya kulelea Watoto yatima, wanaoishi katika mazingira magumu pamoja na Wazee wasiojiweza, Mkurugenzi wetu kwa kutambua makundi haya yaliyopo katika Manispaa yake, ameona ni vyema akayakumbuka kwa kuyapatia ndoo za kunawia mikono, mabeseni pamoja na sabuni za kunawia katika kipindi hiki cha mapambano dhidi ya Virusi vya CORONA, amekuwa akishirikiana vyema na makundi haya katika kutoa misaada mbalimbali pamoja na huduma lakini hili alilolifanya leo ni jambo jema katika kuhakikisha wananchi hawa wanakuwa salama dhidi ya Ugonjwa huu”Amesema Sidina.



Kwa upande wa Mfawidhi wa Makazi ya Wazee wasiojiweza Funga funga, Bi.Rehema Kombe, amemshukuru sana Mkurugenzi wa Manispaa kwa jitihada zake za kuwajali Wazee hao.



“Tunamshukuru sana Mkurugenzi wetu, ameonyesha ni jinsi gani anavyojali afya za Wananchi wake, nakumbuka hii sio mara ya kwanza kutusaidia katika Makao yetu , alishawahi kutupatia TV pamoja na King’amuzi kwa gharama zake na upendo wake, kikubwa tunazidi kumuombea kwa Mwenyezi Mungu ambariki kwa kile alichokitoa hakika tumepata Mama anaye tujali, kwa kutambua mchango wake pongezi hizi hazitaishia kwa maneno pekee bali tutamwandikia barua ya shukrani kwa jinsi anavyozidi kujitoa na kuonyesha upendo kwetu na kuwatia faraja Wazee hawa”Amesema Kombe.



Naye, Mlezi wa kituo cha kulea watoto Mgolole, Sister Palagia Maria , amesema alichokionyesha Mkurugenzi ni upendo kwa Watoto na kuwajali katika afya zao dhdi ya mapambano ya Virusi vya CORONA.



“Mkurugenzi wetu amekuwa akijitoa sana, hivi karibuni akiambatana na Mkuu wa Wilaya wa Morogoro Mhe. Regina Chonjo , walishawahi kuja hapa wakatupatia msaada wa Vyakula ,hivyo huu ni mwendelezo wa kutuunga mkono na tunamuomba aendelee kututhamini na kutusaidia asichoke yeye ni Mama yetu tunapokwama anatakiwa atukwamue, hiki sio kidogo amejinyima na familia yake na kuja kutuletea hapa tunampongeza sana na kumtakia majukumu mema ya kazi zake na kuifanya Manispaa yetu kupiga hatua zaidi za Maendeleo”” Amesema Sister Parakia.



Naye Mwenyekiti wa Wazee hao, Mzee Joseph Kaniki, amemshukuru Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro kwa kuwajali na kuwathamini katika kipindi hiki cha mapambano ya Virusi vya CORONA.



Katika hatua nyengine, Sidina, amesema huu ni mwanzo , hivyo Mkurugenzi amejipanga na timu yake ya Wataalamu wa Afya kwa kushirikiana na Uongozi wa Wilaya ya Morogoro, chini ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Mhe. Regina Chonjo kuhakikisha elimu ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya Virusi vya CORONA inatolewa kila kona katika kulinda hali za afya za Wananchi wao.



Miongoni mwa Makao yaliyopatiwa ndoo, sabuni na mabaseni ni pamoja na Makao ya kulelea Watoto Mgolole, Makao ya kulelea Wazee wasiojiweza Funga funga, Raya, Agape Children’s Village, Dar-Ul- Muslimeen , Mission To The Homeless Children.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa