• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MKURUGENZI MANISPAA YA MOROGORO AWATAKA WANANCHI KUTUMIA FURSA YA MIKOPO KUJIENDELEZA KIUCHUMI.

Posted on: March 12th, 2021

Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, amewataka wananchi wa Manispaa ya Morogoro kutumia fursa ya mikopo kujiendeleza kiuchumi.

Kauli hiyo ameitoa leo Machi 12/2021 ikiwa ni siku moja kupita tangia kufanyika kwa Mkutano wa kujadili mapendekezo ya bajeti  ya mwaka wa fedha 2021/2022 akiwa katika ziara aliyoambatana na Wakuu wa Idara wa Manispaa ya Morogoro ya kukagua baadhi ya vikundi vya vilivyokopeshwa mikopo ya asilimia 10.

Akizungumza na waandishi wa habari, amesema kuwa Manispaa ya Morogoro inaendelea kuwawezesha wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu ili kuweza kujiinua kiuchumi na itawasimamia katika kuhakikisha kuwa mikopo hiyo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu inawanufaisha Wananchi.

" Naahidi kuendelea kuwaendeleza wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu kiuchumi kwa kuwashika mikono kwa kutoa mikopo ya asilimia kumi katika mapato ya ndani, kupitia idara ya maendeleo ya jamii nitaendelea kuwainua wananchi wa Manispaa ya Morogoro , lakini niwaombe hizo fedha mnazokopeshwa ziwe katika mzunguko na zirudishwe kwa wakati ili wengine wapate" Amesema Lukuba.

Aidha Lukuba, amesema kuwa , mikopo hiyo sio zawadi inayotolewa kwao bali wanatakiwa kurejesha kwa wakati ili kuongeza wigo wa utoaji mkopo kwa vikundi vingine vingi zaidi na kukuza uchumi wa wananchi kwa vikundi na mtu mmoja mmoja.

Katika hatua nyingine, Lukuba, amesema kuwa kwa mwaka huu wa fedha 2021/2022 Manispaa ya Morogoro imetenga kiasi cha zaidi ya Tshs.963,000,000.00 kwa ajili ya mikopo ya Wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu. .

Katika ziara ya leo, Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro kwa kushirikiana na Wakuu wa idara wametembelea madarasa 4 yaliyojengwa na TASAF kwa kila shule kwa shule mbili za Sekondari ikiwamo Shule ya Sekondari SUA na Mafiga pamoja na kuangalia ujenzi wa Shule Sekondari SUA .

Lakini pia ukaguzi wa Kikundi kazi cha ndani kilichopata tenda ya uzoaji wa takataka kupitia mkopo wa Manispaa cha M2 Smart , Kikundi cha ujasiriamali wa kushona Masweta cha Kasi Mpya na Silc Kata ya Kihonda, Duka la huduma za kifedha na bidhaa za vyakula la watu wenye ulemavu lililopo Stendi ya Mabasi Msamvu ikiwa na lengo la kuona maendeleo ya vikundi hivyo na kuona kama fedha walizopewa zimetumika kwa malengo yaliyotarajiwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa