• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MKURUGENZI WA MANISPAA AFUNGA BIASHARA ZA VYAKULA KWENYE MAENEO HATARISHI

Posted on: February 16th, 2024


Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro ndugu Ally Machela, ameagiza wananchi wote wenye biashara za kupika na kuuza chakula, waliko kwenye maeneo hatarishi wafunge biashara hizo mara moja ili kuendelea kuwakinga wananchi dhidhi ya ugonjwa wa  kipindupindu ambao athari zake zimeanza kuonekana kwenye baadhi ya maeneo ya Manispaa hiyo ikiwemo kata ya Mafisa.

Ndugu Machela ametoa agizo hilo alipokuwa akijibu hoja za wananchi kwenye mkutano wa hadhara wa Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, wa kusikiliza na kujibu kero za wananchi uliofanyika kwenye mtaa wa Mambi kata ya Mafisa, tarehe 14.02.2024, ambapo amesema mpaka sasa wagonjwa zaidi ya 20 wenye kipindupindu kutoka kata ya Mafisa wanaendelea kupewa matibabu kwenye kitup cha afya cha Mazimbu huku wengine hali zao ziliimarika na wakaruhusiwa kurudi kwenye makazi yao.

“Hatuwezi kuacha wananchi wetu wafe kwa kisingizio cha maisha magumu. Hatuwezi kukubali mtu aendelee na biashara ya kupika na kuuza chakula kwenye maeneo yasiyo sahihi halafu wananchi wetu wakadhurika. Tutaendelea kupita kila siku na kufunga maeneo yote ambayo biashara hizo zinafanyika, mpaka ugonjwa huu upite” alisisitiza Machela.

“Eneo hili ndio ambalo mpaka sasa bado hatujafanikiwa kulidhibiti dhidi ya ugonjwa huu. Ndio maana hadi leo bado mnawaona maafisa afya wetu wanazunguka kwenye mitaa yenu wakitoa vidonge vya kutakasa maji, wakitibu vyanzo vya maji na kutoa elimu ya kujikinga na ugonjwa huu” aliongeza kusema.

Mkurugenzi Machela pia alizungumzia suala la mto Morogoro kuhama na kusababisha maji yake kuathiri sana wananchi wa kata hiyo ya Mafisa ambapo amewataka wananchi waendelee kuwa na subira kwani hivi karibuni wataalamu wa bonde la mto ruvu watapita kwenye maeneo yote na kuweka alama mahali pote ambapo mto huo umechepuka ili waweze kuurudisha katika njia yake.

Vilevile, ndugu Machela amewataka wananchi wa Mafisa wafahamu kwamba uwepo wa dampo la taka ngumu na dampo la maji taka ndani ya kata hiyo ni kwa mujibu wa mipangomiji, hata hivyo kutokana na mji kukua na idadi ya watu kuongezeka na madampo hayo kuanza kuonekana kuwa ni kero kwa wananchi, Manispaa inajipanga kuhakikisha taka ngumu hazitupwi kienyeji kwenye dampo la taka ngumu na kwa upande wa dampo la maji taka, MORUWASA nao wamepata eneo kubwa zaidi huko Kiegea kwa ajili ya kumwaga maji taka. Hivyo taratibu zitakapokamilika dampo la maji taka litaelekezewa huko.

MWISHO


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa