• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MUGAMBI AWASHAURI WATOTO WA KIKE KUVAA MAGAUNI 4 ILI KUTIMIZA NDOTO ZAO

Posted on: May 24th, 2022

AFISA Maendeleo ya Jamii na mratibu wa dawati la maendeleo ya watoto Manispaa ya Morogoro, Joyce Mugambi, amewataka wanafunzi wa kike kuvaa magauni manne ili waweze kutimiza ndoto zao.

Kauli hiyo, ameitoa  katika hafla ya ugawaji wa taulo za mtoto wa kike zilizotolewa na Taasisi ya WEZESHA MABADILIKO kwa wanafunzi wa sekondari wanaoishi katika mazingira magumu katika ukumbi wa mikutano wa  Kilakala uliopo Soko Kuu la Chifu Kingalu Morogoro.

Akizungumza mara baada ya ugawaji wa taulo hizo, Mugambi, amesema kuwa wanafunzi wanatakiwa kusoma kwa bidii ili wafikie malengo ikiwamo magauni manne ambayo ni sare za shule, sherehe za kuagwa za kimasomo ya elimu ya Juu (graduation), Harusi pamoja na wanapoingia katika majukumu ya kifamilia ya kuwa mama ambayo ndio hatua ya mwisho wa kufikia ndoto zake.

Mugambi, amewasihi wanafunzi wasiruke hayo magauni wakaharakia kuvaa magauni kwa kuvuka hatua za uvaaji wa magauni hayo jambo ambalo litawapaelekea kutofikia malengo waliojiwekea.

“ Leo mmeona jinsi watu wanavyotambua umuhimu wenu, nanyi mnatakiwa msome kwa bidii haya magauni mkayavae kwa hatua msiruke hata hatua moja, ukiruka hatua basi ujue unakwenda kubaya, someni kwa bidii mfike chuo kikuu, mfanye sherehe zenu kama wasomi, baaada ya hapo mtaingia katika hatua ya kuwa na familia yaani ndoa kwa kupata mtu ambaye atakuwa chaguo lako na baada ya hapo utapata familia yako hapo utakuwa umekamilisha safari ya mafanikio yako” Amesema Mugambi.

“Tungehitaji kuona wanafunzi wa kike katika Manispaa yetu ya Morogoro wanajitambua, tusingehitaji kuwa na wanafunzi wa kike wanaopata mimba wakakatisha masomo yao na ndoto zao, natamani watoto wa kike wa Manispaa yetu ya Morogoro suala la elimu liwe Kipaumbele chao cha kwanza” Ameongeza Mugambi.

Kwa upande wa Mkuugenzi wa WEZESHA MABADILIKO, Dr. Lusako Mwakiluma,amewaomba walimu kuwasaidia wanafunzi wa kike katika elimu ya kujitambua ili iwasaidie kuepukana na vishawishi vinavyoweza kupekelekea mimba za utotoni.

Dr. Lusako, amesema si masuala yote ya yanayohusu maisha yamewekwa katika mitaala, hivyo walimu wanapaswa kusimama katika nafasi zao kama wazazi ili kile wanachotamani kuwafundisha watoto wao au ndugu zao kwa lengo la kuwalinda na tabia zisizofaa, wakifanye pia kwa wanafunzi wao wa kike ili wawasaidie wasiharibike

Naye Mkaguzi masaidizi wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro, Inspekta Mwanaidi Lwena, ametoa wito kwa watoto wa kike kutokubali kutumiwa kama mitaji na wazazi wao kwa kukatishwa masomo na kuozeshwa mapema, ili kukabiliana na changamoto ya mimba za utotoni katika kufikia ndoto zao.

Inspekta Mwanaidi, amesema walimu wa kike wakiwasaidia na kuwa marafiki kwa watoto wa kike ni rahisi watoto kuwaeleza matatizo yanayowakabili na amewataka wanafunzi kuwa wazi kwa walimu wao wa kike ili wasaidiwe.

Katika hatua nyingine wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mwembesongo Kidato cha 3, Neema Anthony, wameiomba Serikali kuona namna ya kuwashirikisha wazazi na walezi wao katika makongamano ambayo yanatumika kutoa elimu ya masuala ya jinsia ili nao wawe na uelewa juu ya masuala hayo na kujua namna ya kuwasaidia watoto wao.

Miongoni mwa shule za Sekondari ambazo wanafunzi wao wamegaiwa taulo za Mtoto wa kike ni Mafiga, Uwanja wa Taifa, Nanenane, Tubuyu, SUA, Kingo, Kihonda Maghorofani, Mwembesongo, Kayenzi pamoja na Uluguru.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa