• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

NAIBU WAZIRI TAMISEMI DR DUGANGE AAHIDI KUFANYA UPANUZI WA MIUNDOMBINU KITUO CHA AFYA SABASABA MANISPAA YA MOROGORO.

Posted on: June 18th, 2021

Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Dkt. Festo Dugange (MB), ameahidi kufanya upanuzi wa miundombinu ya wodi katika Kituo cha afya cha Sabasaba kilichopo Manispaa ya Morogoro.

Kauli hiyo ameitoa leo Juni 18/2021 wakati wa ziara yake ya kushtukiza katika Kituo hicho cha afya.

Akizungumza na Waandishi wa habari, Dr Dugange, amesema ipo haja ya kituo hicho cha afya kuongezewa miundombinu ya wodi ili hata wananchi wakifika kupata huduma wapate sehemu za kulazwa kwani bado kituo hicho kina eneo la kutosha.

Dr Dugange, amesema kuwa atahakikisha suala hilo analifikisha Wizarani ili kuona ni kwa namna gani anaweza kuona miundombinu hiyo inakamilika hata kwa kuanzia kwa ujenzi wa awamu kwa awamu lengo ni kupata wodi ya kulazwa wagonjwa.

Katika hatua nyingine, Dr Dugange, ameupongeza uongozi wa Kituo cha afya chini ya Mganga mfawidhi wa kituo hicho kwa kufanya vizuri katika eneo la makusanyo ya fedha kupitia mifuko ya afya ikiwemo NHIF , CHF, pamoja na uuzaji wa dawa na huduma nyingine.

"Naamini kabisa mnanafasi kubwa ya kuendelea kukusanya fedha zaidi ya hizi mnazo kusanya kwa sasa kama mkijipanga vizuri, kwa sababu nyinyi kwa wastani kwa mwezi mnakusanya milioni 12 sawa na ukusanyaji wa shilingi 400,000/= kwa siku, kwahiyo ukijumlisha fedha za NHIF milioni 4, CHF milioni 2 na zile milioni 12 ambazo hazihusiani na mifuko hii ya afya mtajikuta mnakusanya milioni 18 kwa mwezi hivyo mnauwezo wa kuboresha mifumo zaidi mkapata kwa mwezi zaidi ya milioni 25 kama mkijipanga vizuri " Amesema Dr Dugange.

Aidha, Dr Dugange, ameutaka Uongozi huo kwa kushirikiana na Manispaa wakae chini waweke mipango mizuri ambayo kwa sasa ni agenda ya kongeza mapato mara mbili ya hapo yanayokusanywa katika Vituo husika .

Amesema kuwa Serikali kwa sasa imedhamiria kuboresha huduma za afya ili vituo vya afya viweze kuongeza wateja wengi zaidi , wateja wasikae muda mrefu kusubiria huduma

Hata hivyo, ameupongeza Uongozi wa Kituo hicho cha afya kwa kuwa na dawa za kutosha na mpangilio mzuri wa bohari ya dawa jambo ambalo linaonesha dalili nzuri ya kupata huduma bora na kuongeza wateja wengi zaidi.

Dr Dugange, ameutaka Uongozi wa Kituo hicho cha afya kuhakikisha kwamba wanashughulikia haraka sana changamoto za vifaa tiba ili viweze kutumika katika kutoa huduma kwa wateja.

Amesema kuwa kuwepo kwa changamoto za vifaa tiba kunawapotezea mapato kutokana na kuwakosa wateja wanaohitaji huduma za vipimo lakini kuna athiri upatikanaji wa huduma kwa wananchi .

Mwisho amemuagiza Mganga Mfawidhi wa Kituo hicho cha afya kuhakikisha wanawahudumia haraka Wazee ili kuendana na dhana ya Serikali ya kuanzisha dawati la kuwahudumia wazee kuliko kuwaacha wazee wakikaa muda mrefu kusubiria huduma.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa