• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

RAS MOROGORO AFUNGA RASMI UMITASHUMTA, ATOA AGIZO KWA WAKURUGENZI

Posted on: May 29th, 2023

KATIBU Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa amefunga mashindano ya Umoja wa michezo kwa shule za msingi Tanzania (UMITASHUMTA) ngazi ya Mkoa huku akiwataka Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa  kusaidia timu zao zinazoshiriki mashindano hayo kwa kuwapatia vifaa vya michezo pamoja na kutoa michango ya ushiriki.

Hafla hiyo ya ufungaji wa mashindano hayo imefanyika Mei 29 mwaka huu katika viwanja vya shule ya Sekondari ya Morogoro iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, ambapo Halmashauri zote 9 za Mkoa huo zimeshiriki kwa kutoa wanamichezo.

Dkt. Mussa amesema kuwa Wakurugenzi wanajukumu la kusaidia wanamichezo wao kwa kutoa michango ikiwemo fedha za ushiriki na vifaa vya michezo kwa mashindano yajayo hivyo wakurugenzi wajipange kikamilifu.

“...lakini mbaya zaidi hata hao wanafunzi wanaokuja kuwakilisha Halmashauri zenu mmeshindwa kuwapa sare nzuri sasa mimi niwaambieni hili sitaki kuliona tena kwenye michezo ijayo...” amesema Dkt. Mussa.

Aidha, Katibu Tawala huyo amesema michezo ina faida nyingi sio kuimarisha afya bali hupanua uwezo wa akili kufikiri, pamoja na kupunguza matukio ya kiharifu kwa sababu watu watatumia muda mwingi kwenye michezo kuliko kukaa vijiweni bila kazi.

Sambamba na hilo Dkt. Mussa amewatakia kila la heri wanamichezo waliochaguliwa kuuwakilisha Mkoa katika Mashindano hayo ngazi ya Taifa yatakayofanyika Juni 2, 2023 Mkoani Tabora na kuahidi kuandaa zawadi endapo timu hiyo itafanya vizuri katika mashindano hayo.

Awali, Afisa Michezo Mkoa wa Morogoro Bi. Grace Njau amesema mashindano hayo yamewakutanisha wanamichezo 938 kutoka Halmashauri zilizopo Mkoa wa Morogoro wakiwemo wavulana 453, wasichana 485 ambao wameshiriki michezo mbalimbali ikiwemo michezo ya riadha, mpira wa miguu, netiboli, mpira wa wavu, kwaya, na muziki.

Bi. Grace ameongeza kuwa mashindano ya mwaka jana Mkoa wa Morogoro ulishika nafasi ya tano kitaifa, pia ulipata Medali nne katika mashindano ya Afrika.

Mashindano hayo kwa mwaka huu yanaenda sambamba na kaulimbiu isemayo “Uimarishaji wa miundombinu ya elimu nchini ni chachu ya taaluma, sanaa na michezo”.

Jumla ya wanamichezo 102 wamechaguliwa kuuwakilisha Mkoa katika mashindano hayo ya UMITASHUMTA ngazi ya taifa Mkoani Tabora ambayo yataanza Juni 2 mwaka huu.




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • DKT.KIJAJI AFUNGA WIKI YA MAZIWA KITAIFA NA KUWATAKA WAFUGAJI KUZALISHA MAZIWA SALAMA KUENDANA NA USHINDANI WA SOKO LA MAZIWA.

    June 02, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA YAO MARA KWA MARA

    May 31, 2025
  • WATENDAJI WA MITAA WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MKATABA WA LISHE

    May 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa